Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Urais Z’bar: 15 warejesha fomu CCM, waliojitosa 30
Habari za Siasa

Urais Z’bar: 15 warejesha fomu CCM, waliojitosa 30

Pereira Ame Silima aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani wa Tanzania
Spread the love

WANACHAMA 15 wa Chama cha Mapinduzi (CCM), wamerudisha fomu ya kugombea Urais wa Zanzibar, katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

CCM ilifungua zoezi la uchukuaji na urejeshaji fomu, sambamba na utafutaji wadhamini 250 kwa kila mtia nia wa kugombea nafasi hiyo, tarehe 15 Juni 2020. Zoezi hilo linatarajiwa kufungwa Jumanne ya tarehe 30 Juni 2020.

Hadi jana Ijumaa tarehe 26 Juni 2020, takribani makada 15 kati ya 30 waliojitokeza kugombea nafasi hiyo, walirejesha fomu za kugombea urais wa Zanzibar.

Wanachama hao wa CCM walizikabidhi fomu zao kwa Cassian Gallo’s , Katibu wa Kamati Maalumu ya NEC, Idara ya Oganaizesheni Zanzibar, kwenye Ofisi Kuu ya chama hicho visiwani humo, iliyoko maeneo ya Kisiwandui.

Waliorudisha fomu ni, Balozi Ali Abeid Karume, mtoto wa Rais Mstaafu wa Zanzibar, Hayati Abeid Amani Karume. Dk. Hussein Mwinyi, Waziri wa Ulinzi na Mtoto wa Rais Mstaafu wa Tanzania, Dk. Ali Hassan Mwinyi.

Wengine ni, Shamsi Vuai Nahodha, aliyekuwa Waziri Kiongozi wa Zanziba. Mhandisi Makame Mbarawa, Waziri wa Maji. Mbwana Bakari Juma, Mbwana Yahya Mwinyi, Omar Shehe Mussa, Mohamed Hijja Mohamed na Mohamed Jumanne.

Issa Suleiman Nassor, Abdulhalim Mohamed Ali, Khamis Mussa Omar, Rashid Ali Juma, Dk. Khalid Salum Mohamed, na Ayoub Mahmoud Mohamed.

Wanachama wengine 15 ambao hajarudisha fomu zao ni, Mussa Aboud Jumbe, Mtoto wa Rais Mstafu wa Zanzibar. Fatma Kombo Masoud, Hasna Atai Masoud, Iddi Hamad Iddi, Pereira Ame Silima, Shaame Simai Mcha, Hashim Salum Hashim na Ayoub Mohammed Mahmoud.

Hasna Atai Masoud

Wengine ni, Hussein Ibrahim Makungu, Bakari Rashid Bakari, Mohammed Aboud Mohammed, Mhandisi Hamad Yusuph Masauni, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani.  Mmanga Mjengo Mjawiri, Khamis Mussa Omar na Rashid Ali Juma.

Wagombea wote 29 waliojitokeza ni;

 

  1. Mbwana Bakari Juma
  2. Balozi Ali Abeid Karume
  3. Mbwana Yahya Mwinyi :
  4. Omar Sheha Mussa
  5. Dk. Hussein Ali Mwinyi
  6. Shamsi Vuai Nahodha
  7. Mohammed Jaffar Jumanne
  8. Mohammed Hijja Mohammed
  9. Issa Suleiman Nassor
  10. Profesa Makame Mnyaa Mabarawa
  11. Mwatum Mussa Sultan
  12. Haji Rashid Pandu
  13. Abdulhalim Mohammed Ali
  14. Jecha Salum Jecha
  15. Dk. Khalid Salum Mohammed
  16. Rashid Ali Juma
  17. Khamis Mussa Omar
  18. Mmanga Mjengo Mjawiri
  19. Hamad Yussuf Masauni
  20. Mohammed Aboud Mohammed
  21. Bakari Rashid Bakari
  22. Hussein Ibrahim Makungu
  23. Ayoub Mohammed Mahmoud
  24. Hashim Salum Hashim
  25. Hasna Atai Masound
  26. Fatma Kombo Masound
  27. Iddi Hamadi Iddi
  28. Pereira Ame Silima
  29. Shaame Simai Mcha
  30. Mussa Aboud Jumbe

Endelea kufuatilia MwanaHALISI ONLINE & MwanaHALISI TV

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

error: Content is protected !!