SHIRIKA la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limewatangazia neema wakulima wa mazao ya chakula nchini, ambapo imewahakikishia kwamba itanunua chakula cha ziada kitakachozalishwa zaidi ya tani milioni 3. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).
Hayo yamesemwa leo terehe 27 Julai, 2018 na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa baada ya kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa WFP, Bw. David Beasley, jijini Dar es Salaam.
Waziri Majaliwa amesema Beasley amemhakikishia kwamba shirika lake litayanunua mazao hayo, na hivyo kupunguza tatizo la ukosefu wa masoko kwa wakulima.
“Taarifa za Wizara ya Kilimo zinaonesha kuwa mavuno ya mazao ya chakula kama mahindi, maharage na mbaazi yatafikia tani milioni 16 wakati mahitaji ya chakula kwa Watanzania kwa mwaka ni tani milioni 13, hivyo tutakuwa na ziada ya tani milioni tatu,” amesema.
Vile vile, Waziri Majaliwa amesema ujio wa Beasley hapa nchini ni fursa itakayowawezesha Watanzania kunufaika kwa kiwango kikubwa katika kilimo, uhifadhi na uuzaji wa mazao ya chakula yanayolimwa hapa nchini.
Leave a comment