Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Umoja wa Mataifa kununua tani mil 3 za chakula
Habari Mchanganyiko

Umoja wa Mataifa kununua tani mil 3 za chakula

Mahindi yakiwa shambani
Spread the love

SHIRIKA la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limewatangazia neema wakulima wa mazao ya chakula nchini, ambapo imewahakikishia kwamba itanunua chakula cha ziada kitakachozalishwa zaidi ya tani milioni 3. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Hayo yamesemwa leo terehe 27 Julai, 2018 na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa baada ya kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa WFP, Bw. David Beasley, jijini Dar es Salaam.

Waziri Majaliwa amesema Beasley amemhakikishia kwamba shirika lake litayanunua mazao hayo, na hivyo kupunguza tatizo la ukosefu wa masoko kwa wakulima.

“Taarifa za Wizara ya Kilimo zinaonesha kuwa mavuno ya mazao ya chakula kama mahindi, maharage na mbaazi yatafikia tani milioni 16 wakati mahitaji ya chakula kwa Watanzania kwa mwaka ni tani milioni 13, hivyo tutakuwa na ziada ya tani milioni tatu,” amesema.

Vile vile, Waziri Majaliwa amesema ujio wa Beasley hapa nchini ni fursa itakayowawezesha Watanzania kunufaika kwa kiwango kikubwa katika kilimo, uhifadhi na uuzaji wa mazao ya chakula yanayolimwa hapa nchini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!