Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli awaapisha viongozi sita Dodoma
Habari za Siasa

Rais Magufuli awaapisha viongozi sita Dodoma

Spread the love

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli leo Alhamisi tarehe 21 Mei 2020 amewaapisha viongozi sita aliowateua hivi karibuni. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Hafla ya kuwaapisha viongozi hao imefanyika katika Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma asubuhi hii.

Viongozi walioapishwa ni; Dk. Godwin Mollel kuwa Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii,Jinsia Wanawake Wazee na Watoto.

Dk. Mollel ameapishwa kuchukua nafasi ya Dk. Faustine Ndungulile ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.

Dk. Delphine Magere ameapishwa kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani kuchukua nafasi ya Theresia Mbando ambaye amestaafu kwa mujibu wa utumishi wa umma.

Wengine ni; Dk. Jacob Kingu kuwa Balozi wa Tanzania nchini Algeria, Phaustine Kasike kuwa Balozi wa Tanzania nchini Msumbiji na John Simbachawene kuwa Balozi wa Tanzania nchini Kenya.

Pia, Rais Magufuli amemwapisha Brigedia Jenerali, John Mbungo kuwa Mkurugenzi mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa (Takukuru).

Hafla hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwamo mawaziri na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI ONLINE kwa habari zaidi 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!