Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Magufuli ateua mwenyekiti mpya TASAC
Habari Mchanganyiko

Rais Magufuli ateua mwenyekiti mpya TASAC

Rais John Magufuli
Spread the love

MKUU wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) Profesa Tadeo Andrew Satta, ameteuliwa na Rais John Magufuli kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Wakala wa Meli Tanzania (TASAC). Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais-Ikulu, Gerson Msigwa, uteuzi wa Prof. Satta umeanza jana tarehe 23 Aprili 2019.

Vile vile, Rais Magufuli ameteua Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa TASAC, akiwemo Daniel Mchome, Mussa Mandia, Evelyne Makala, Renatus Mkinga, Japhet Massele na Bernard Asubisye.

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli amemteua Emmanuel Ndomba kuwa Mkurugenzi Mkuu wa TASAC.
“Uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TASAC, Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya TASAC na Mkurugenzi wa TASAC umeanza leo (jana) tarehe 23 Aprili 2019,” inaeleza sehemu ya taarifa ya Msigwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!