Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli amtaka Ney wa Mitego aboreshe ‘Wapo’
Habari za SiasaMichezoTangulizi

Rais Magufuli amtaka Ney wa Mitego aboreshe ‘Wapo’

John Magufuli, Rais wa Tanzania
Spread the love

JOHN Magufuli, Rais wa Tanzania, ameliagiza Jeshi la Polisi kumwachia huru msanii wa muziki wa kizazi kipya, Emmanuel Eribariki ‘Nay wa Mitego’ huku akimshauri kuporesha wimbo wake wa Wapo, anaandika Faki Sosi.

Ney wa Mitego alikamatwa na polisi mkoani Morogoro juzi usiku na kuleta jijini Dar es Salaam kwa madai ya kuimba wimbo uliokuwa na maneno yanayoikashifu serikali na viongozi wake.

Rais Magufuli kupitia kwa Dk. Harrison Mwakyembe, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa, Michezo, aliwaeleza waandishi wa habari kuwa Rais Magufuli amevutiwa na wimbo huo kutokana na kueleza hali halisi na kwamba ameshauri kuwa wimbo huo ungeendelezwa klwa kuwataja wakwepa kodi, wauzaji na watumiaji wa dawa za kulevya, na watu wanaofanya mambo yasiyofaa katika jamii.

Dk. Mwakyembe alidai kuwa Rais alimuambia kuwa: “Huyo kijana wako (Ney) aboreshe huo wimbo asiondoe chochote ila angoze aileze changamoto za jamii halafu aitike kama ulivyo wimbo wenye ‘wapo’… wauza madawa ya kulevya wapo… wakwepa kodi wapo…” alidai Dk Mwakyembe .

Dk  Mwakyembe alikiri kuwa alishauriwa na Baraza la Sanaa Tanzania (Basata) kuhusu wimbo huo na kwamba aliwaambia wauwachie.

Baadhi ya mashairi yaliyokuwepo kwenye wimbo huo , “Hivi Uhuru wa Kuongea bado upo? Siamini nchi inaendeshwa kwa kiki! Nasikia kuna viongozi wamefoji vyeti? Wapooo! Mheshimiwa hivi unamjua Bashite kutoka Kolomije? We si Dokta wa kutumbua majipu?”

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

error: Content is protected !!