BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA), limesema mwaka huu hakutakuwa na ibada ya Hijja, kutokana na janga la Virusi vya Corona. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).
Kauli hiyo imetolewa leo Alhamisi tarehe 25 Juni 2020 na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zubeir Ally wakati anazungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam.
Mufti Zubeir amesema, hatua hiyo imetokana na zuio lililotolewa na nchi ya Saudi Arabia, kwa waumini wa Dini ya Kiislamu kutoka nje ya nchi hiyo, kufanya ibada hiyo, ili kudhibiti maambukizi ya Ugonjwa wa Homa Kali ya Mapafu, inayosababishwa na Virusi vya corona (Covid-19).
Sambamba na hilo, Mufti Zubeir ameagiza madrasa zote nchini kufungulia kuanzia leo, huku akiwataka viongozi wa madrasa hizo, kufuata taratibu zote za kiafya, kwa ajili ya kujikinga na Covid-19.
Agizo hilo la kufunguliwa kwa madrasa, limekuja baada ya Rais John Magufuli, kuagiza shule zote nchini, kufunguliwa kuanzia Jumatatu ya tarehe 29 Juni 2020.
Leave a comment