Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mkurugenzi Jamii Forum ahukumiwa
Habari Mchanganyiko

Mkurugenzi Jamii Forum ahukumiwa

Maxence Melo
Spread the love

MAXENCE Melo, Mkurugenzi wa Mtandao wa Jamii Forums,  amehukumiwa kutotenda kosa la kuzuia Jeshi la Polisi kutekeleza wajibu wao kwa mwaka mmoja. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Hukumu hiyo imetolewa leo tarehe 17 Novemba 2020 na Huruma Shaidi, Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu, jijini Dar es Salaam baada ya kumkuta na hatia katika shitaka lake la kuzuia upelelezi wa Jeshi la Polisi.

Wakati akitoa hukumu ya kesi hiyo namba 458 ya mwaka 2016, iliyokuwa inamkabili Melo na mwenzake Mike Mushi, Huruma Shaidi amesema mahakama imemuacha huru Melo kwa masharti ya kutofanya kosa kama hilo ndani ya mwaka mmoja.  Mushi hakukutwa  na hatia yoyote.

Katika kesi hiyo, Melo na Mushi walikuwa wanakabiliwa na mashtaka mawili, kuendesha mtandao ambao haujasajiliwa kwa kikoa cha Tanzania (.Tz) na kuzuia upelelezi wa Jeshi la Polisi.

Ambapo, Melo alikutwa na hatia katika shitaka la kuzuia Upelelezi wa Jeshi la Polisi huku mwenzake akikutwa hana hatia katika mashtaka yote mawili.

Katika kesi hiyo, Melo alikuwa akituhumiwa kutotoa taarifa kwa Jeshi la Polisi kuhusu wanachama wawili wa Jamii Forums waliodaiwa kuandika madai ya uhalifu uliotuhumiwa kufanywa na benki ya CRDB kwa kushirikiana na wafanyakazi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!