Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mbaroni kwa kujiteka jijini Mwanza
Habari Mchanganyiko

Mbaroni kwa kujiteka jijini Mwanza

Spread the love

Mfanyabiashara Prosper Peniel (26) mkazi wa Kwimba mkoani Mwanza anashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani humo kwa kosa la kutoa taarifa ya uongo kuwa ametekwa na watu wasiojulikana kwa lengo la kuishinikiza familia yake imtumie kiasi cha Sh. milioni 53. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 02 Agosti, 2018 na  Kamanda wa Polisi Mwanza, DCP Ahmed Msangi, ambapo amesema mtuhumiwa huyo alisambaza taarifa hizo tarehe 18 Agosti mwaka huu.

Kamanda Msangi amesema Peniel aliwataka ndugu zake kumtumia kiasi hicho cha fedha ili aachiwe kitendo ambacho ni kosa la jinai.

“Mtuhumiwa alimtumia ndugu yake ujumbe mfupi kupitia simu yake ya mkononi kuwa ametekwa na watu wasiojulikana wakati akitembea kwa miguu katika barabara ya Kenyatta karibu na jengo la NSSF plaza hapa jijini mwanza. Baada ya ndugu zake kupokea taarifa hizo walitoa taarifa kituo cha polisi,” amesema Kamanda Msangi na kuongeza.

“Askari kwa kushirikiana na ndugu wa mtuhumiwa walianza kufanya ufuatiliaji katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Mwanza na maeneo ya mikoa ya jirani ili kuweza kubaini wahusika waliomteka mtuhumiwa na mahala alipopelekwa baada ya kutekwa.

“Ndipo tarehe tajwa hapo juu polisi walifanikiwa kumkamata mtuhumiwa akiwa amelala kwenye nyumba ya  kulala wageni ya majani lodge iliyopo wilayani Kwimba  akiwa na simu ya mkononi aliyokuwa akiitumia kutoa taarifa za uongo kwa ndugu na marafiki kuwa ametekwa.”

Kamanda Msangi amesema Polisi wapo katika upelelezi na mahojiano na mtuhumiwa, na kwamba pindi uchunguzi ukikamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani. Aidha uchunguzi zaidi kuhusiana na tukio hilo bado unaendelea.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!