Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Kesi ya Manji yapigwa kalenda
Habari Mchanganyiko

Kesi ya Manji yapigwa kalenda

Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam imeahirisha kesi inayomkabili Yusuph Manji, Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga, anaandika Hamisi Mguta.

Manji ambaye pia ni mfanyabiashara maarufu hapa nchini anakabiliwa na kesi ya kukutwa na sare za Jeshi la Wananchi wa Tanzania pamoja na mihuri kadhaa ya jeshi hilo kinyume cha sheria.

Kesi hiyo iliyopangwa kusikilizwa leo, haikusikilizwa kutokana na mahakama kuambiwa kwamba upelelezi wake haujakamilika.

Aidha, jana mtuhumiwa huyo alikwama kufika mahakamani hapo kwa madai kwamba ni mgonjwa na anadaiwa kupelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Madai hayo ya Manji kuumwa yametolewa leo katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam na wakili wake.

Kesi ya mfanyabiashara huyo imepangwa kusikilizwa Agost 4, mwaka huu.

Manji alisomewa mashtaka saba Julai 5 mwaka huu akiwa amelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na watuhumiwa wenzake, kwa makosa ya uhujumu uchumi, kukutwa na mihuri miwili ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!