Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko JWTZ wawaita madaktari kujiunga na jeshi
Habari Mchanganyiko

JWTZ wawaita madaktari kujiunga na jeshi

Msemaji Mkuu wa JWTZ, Kanali Ramadhani Dogoli
Spread the love

JESHI la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limetangaza nafasi za kuandikishwa jeshini madaktari wa binadamu na fani nyingine za tiba. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 31, 2018 na Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano JWTZ, Kanali Ramadhan Dogoli wakati akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam.

“Nafasi hizo zinatolewa ili kuongeza idadi ya wataalamu wa tiba watakaotoa huduma za afya katika hospitali zetu, vituo vya afya na Zahanati kulingana na mahitaji ya sasa na siku zijazo,” amesema Kanali Dogoli.

Kanali Dogoli ametaja sifa za watu wanaohitajika kuandikishwa ikiwemo, mhusika awe na umri kati ya miaka 18 hadi 28 na mzaliwa wa Tanzania, awe hajawahi kupatikana na hatia ya makosa ya jinai mahakamani na kufungwa jela, awe na cheti halisi cha kuziliwa.

Pia, kama ni daktari awe amemaliza mafunzo kwa vitendo na kutunukiwa vyeti pamoja na kusajiliwa na Bodi. Awe hajawahi kutumikia Jeshi la Polisi, Magereza, Chuo cha Mafunzo au Kikosi Maalumu cha Kuzuia Magendo.

Kanali Dogoli amesema   wenye sifa tajwa na kuhitaji kujiunga na JWTZ waripoti katika kambi ya Jenerali Abdallah Twalipo, Mgulani Dar es Salaam tarehe 28 Agosti, 2018 kuanzia saa moja asubuhi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!