SERIKALI imesema itapanga bei elekezi ya madini ili kundoa urasimu wanaofanyiwa wachimbaji wadogo wakati wa uuzaji. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).
Hayo yalisemwa jana na Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula alipotembelea kijiji cha Manda kilichopo Wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma ambapo kunachimbwa madini ya jasi (Gypsum).
“Kijiji cha Manda changamoto kubwa ni soko la gypsum, inaonekana wazi wachimbaji wanawaonewa kuna watu wanwalalia. Tumepanga tume tukae pamoja tutengeneze, tuziweke bei elekezi ili wanao nunua madini wafuate bei hizo.
“Sababu watu wetu wamewekeza kwenye madini hayo tumekuta malundo ya Gypsum yako sokoni bei wanayoambiwa watanunua hairidhishi,” alisema Pro. Kikula.
Prof. Kikula aliongeza kuwa “Hiyo hiyo gypsum inanunuliwa Itigi kwenda Mtwara kwa bei ya kutupwa, wananchi wanapata shida wanasafirisha kwa bei ndogo. Tutatengeneza bei elekezi ili iwe kigezo cha ununuzi na uuzaji wa madini sokoni.”
Katika hatua nyingine, Prof. Kikula aliwataka wachimbaji wadogo kuheshimu mamlaka za maeneo wanayochimba madini ikiwa pamoja na kuwa na mahusiano mazuri na viongozi wa serikali husika ili kuepusha migogoro.
“Katika ziara yetu tumekwenda kujua matatizo ya uchimbaji, tumekwenda Manzase njia ya kutoka Dodoma hadi Iringa kabla ya kuzungumza na wachimbaji tumezungumza na serikali ya kijiji kuhusu uchimbaji.
Wachimbaji lazima waheshimu mamlaka ya maeneo wanayochimba bila ya kuwa na mahusiano mazuri kunaleta migogoro,” alisema.
Leave a comment