Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Michezo Dakika ya 87 yamvuruga Samatta
Michezo

Dakika ya 87 yamvuruga Samatta

Spread the love

BAO lililofungwa katika dakika ya 87 na Theo Walcott, mchezaji wa Klabu ya Everton katika mechi ya Ligi Kuu Uingereza (EPL), limezamisha ndoto ya mchezi wa kimataifa wa Tanzania anayechezea Klabu ya Aston Villa, Mbwana Samatta kubaki EPL msimu ujao. Inaripoti mtanda wa habari wa BBC…(endelea).

Walcott ameongeza mzigo kwa Samatta na klabu yake kwamba, ili iweze kucheza EPL, basi klabu hiyo inapaswa kushinda mechi zake mbili zilizosalia kati yake na Arsenal pia West Ham, vinginevyo msimu ujao watausikia kwenye bomba.

Villa ambayo ilikuwa ugenini, ilipigana kufa kupona ili itoke na ushindi na hatimaye kuinua manumaini ya kubaki EPL msimu ujao, bao la Ezri Konsa katika uwanja wa Everton – Goodison Park – liliongeza ari kwa Villa.

Kwa sasa Villa ipo katika nafasi ya 19 EPL, ina pointi nne nyuma ya Watford, ambayo inashikilia nafasi ya mwisho juu ya eneo la kushushwa daraja.

Arsenal ambayo hivi karibuni iliwatandika mabingwa Liverpool, inaonekana kuimarika huku wakiwa na matumaini ya kushinda mechi mbili zilizosalia ikiwemo ya Aston Villa.

West ham ambayo ipo katika nafasi ya 16 na haijacheza mechi moja, iko pointi sawa na Watford na inatishiwa kushuka daraja iwapo itapoteza mechi tatu zilizosalia.

Mashabiki wa Villa pia watakuwa wakiangalia matokeo ya klabu ya Bounemouth, Watford na West Ham katika wiki zijazo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!