Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Corona: Tanzania kuingia hatua ngumu
AfyaHabari MchanganyikoTangulizi

Corona: Tanzania kuingia hatua ngumu

Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya
Spread the love

WATANZANIA wametakiwa kuongeza umakini katika kujilinda na virusi vya corona (COVID-19), kwa kuwa siku chache zijazo, nchi itaingia katika hatua ya kuambukizana wenyewe kwa wenyewe. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam …(endelea).

Na kwamba, katika hatua hiyo, mtua anaweza kupata maambukizi na asijue amepata kutoka wapi.  

Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya akifungua mkutano wa viongozi wa madhehebu ya dini kitaifa leo tarehe 9 Aprili 2020, amesema maambukizi kutoka nje (imported transmition) yamedhibitiwa.

“Tumetoka kwenye maambukizi yanayoletwa kutoka nje ya nchi (imported transmission), tuko kwenye local transmission (maambukizi ya ndani). Hivi sasa, takwimu za kesi za jana na juzi, zinaonesha tumeanza kuambukizana wenyewe kwa wenyewe, hili lazima tuweke wazi. Hakuna maambukizi ya nje,” amesema Waziri Ummy na kuongeza:

“Tumeanza kwenye ‘local transmission’ na siku chache tutaingia kwenye ‘community transmission,’ maana yake tutapata mgonjwa hatutajua ameupata wapi huo ugonjwa, ndio maana tunafanya ufuatiliaji.

“Na ndani ya siku chache tutaingia katika hatua hiyo, lazima niwaambie ukweli viongozi wa dini, nisiwafiche kwamba soon tutaingia kwenye community transmission.”

Hata hivyo, Waziri Ummy amesema Tanzania imevuka kihunzi cha Shirika la Afya la Kimataifa (WHO), cha kuwa na wagonjwa 1,000 wa COVID-19 ifikapo katikati ya mwezi Aprili mwaka huu.

“Tunamshukuru Mungu, hadi sasa anatutendea maajabu, tumevuka kihunzi WHO, walisema mwezi Aprili tutapata wagonjwa 1,000 na kati kati ya mwezi Mei tutapata wagonjwa 10,000 lakini kila mtu akichukua nafasi yake, tunaweza kuvuka hicho walichotutabiria,” amesema Waziri Ummy.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Afya

Mloganzila yajipanga kupandikizaji wa ini

Spread the love  HOSPITALI ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imesema kutokana na uwekezaji uliofanywa...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

error: Content is protected !!