Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa NCCR- Mageuzi yakana madai ya ‘Shangazi’
Habari za SiasaTangulizi

NCCR- Mageuzi yakana madai ya ‘Shangazi’

Spread the love

CHAMA cha NCCR- Mageuzi, kimekana madai kuwa kimetumia kiasi Sh. 1.19 bilioni, zilizotolewa na serikali, bila kuwa na uthibitisho wa nyaraka. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Katibu mkuu wa chama hicho, Elizabeth Mhagama amesema, chama chake kinapokea ruzuku ya chini ya Sh. 3.5 milioni kwa mwezi, na hivyo, kwa vyovyote vile, “hakiwezi kutumia mabilioni hayo ya shilingi.”

Mhagama ametoa kauli hiyo, katika mahojiano yake na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu jana Jumatano. Alikuwa akijibu madai yaliyokuwa yametolewa na wakili mashuhuri wa mahakama kuu, Fatma Karume.

Akiandika katika ukurasa wake wa twitter, Fatma ambaye anafahamika pia kwa jina la Shangazi amekituhumu chama hicho, kwa kile alichodai, “matumizi mabaya ya fedha za umma.”

Amesema, “sikuweza kustahimili mpaka kesho. NCCR- Mageuzi na CUF (Chama cha Wananchi), wamepewa adverse (reports – report mbaya) na CAG (Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa hesabu za Serikali).”

Anaongeza: Sababu, NCCR wametumia zaidi ya Sh. 1.19 bilioni, bila kuwa na uthibitisho. Nayo CUF pia hawana vithibitisho ya matumizi ya zaidi ya Sh. 580. Wache waunge mikono juhudi tu.”

Kwa mujibu wa ripoti ya CAG inayoeleza hali ya vyama vya siasa, chama cha NCCR- Mageuzi, tofauti na anavyoeleza Fatma Karume, chama hicho, kimetumia kiasia cha Sh. 1,190,250 tu.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!