Sunday , 7 July 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Waingereza kuifuta historia ya Conservatives leo?
Habari za SiasaKimataifa

Waingereza kuifuta historia ya Conservatives leo?

Waziri mkuu wa Uingereza, Rishi Sunak.
Spread the love

Waingereza milioni 50 wanatarajiwa kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu leo Alhamisi, huku kiongozi wa chama cha upinzani cha Labour akitabiriwa kumbwaga waziri mkuu wa sasa, Rishi Sunak, baada ya miaka 14 ya utawala wa chama cha Conservatives. Inaripoti Mitandao ya Kimataida … (endelea).

Uchunguzi wa maoni ya wapigakura unaonesha kwamba Keir Starmer wa Labour atapata ushindi mkubwa kutokana na wapigakura kuchoshwa na wahafidhina, ambao wameonesha kiwango cha juu cha mgawanyiko uliosababisha Uingereza kuwa na mawaziri wakuu watano ndani ya kipindi cha miaka minane.

Keir Starmer

Hata hivyo, uchunguzi huo wa maoni unaonesha kuwa wapigakura wanataka mabadiliko, na sio kwamba wanakiunga mkono chama cha Labour, kinachofuata siasa za mrengo wa kati kushoto.

Kwenye taarifa yake iliyotolewa leo, Starmer amewaambia wapigakura kwamba huenda leo, Uingereza ikaanza ukurasa mpya, lakini amewaonya kuwa hilo litawezekana tu endapo watajitokeza kwa wingi kupiga kura.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Mwabukusi aenguliwa Urais TLS, mwenyewe agoma

Spread the loveKAMATI ya Rufaa ya Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), imemuengua...

Habari za SiasaKimataifa

Starmer atangaza baraza jipya la mawaziri UK

Spread the loveKufuatia ushindi wa kishindo ambao chama cha Labour kimeupata katika...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Bodi ya sukari, wazalishaji jino kwa jino

Spread the loveMVUTANO wa utoaji wa vibali za sukari na nakisi umeendelea...

error: Content is protected !!