Sunday , 30 June 2024
Home Kitengo Biashara Wafanyabiashara Kagera, Morogoro nao wagoma, Songwe wakimbilia Zambia
BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara Kagera, Morogoro nao wagoma, Songwe wakimbilia Zambia

Spread the love

MGOMO wa wafanyabiashara kutoka katika mikoa mbalimbali nchini imendelea kushika kasi baada ya mikoa ya Morogoro na Kagera kuungana na wengine wa mikoa nane kutofungua maduka yao.

Aidha, kwa upande wa Songwe wafanyabiashara na wananchi wa mji wa kibiashara wa Tunduma nao wamehamia upande wa pili wa nchi jirani ya Zambia ili kupata huduma. Anaripoti Ibrahim Yassin, Songwe…(endelea).

Baadhi ya maduka halmashauri ya mji Tunduma yakiwa yamefungwa.

Akizungumza na MwanaHALISI leo Alhamisi, Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanyabiashara bidhaa za Viwanda na Kilimo (TCCIA) wilayani Momba, Peter Mwamboneke amesema wanahitaji kodi rafiki sio kandamizi hasa ikizingatiwa mitaji yao inatokana na mikopo kutoka kwenye taasisi na benki mbalimbali.

“Asilimia 75 ya wafanyabiashara wenye maduka upande wa Nakonde nchini Zambia ni watanzania ambao wamekimbilia huko kufuata nafuu ya kodi na tozo” amesema Mwamboneke.

Mwenyekiti huyo ameongeza kuwa wao ni wazalendo hawakutaka kukimbilia upande wa Zambia licha ya kuwa kunahuduma zote lakini wanaiomba serikali iangalie kwa jicho la tatu utatuzi wa changamoto za wafanyabiashara.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Mpina amng’ang’ania Bashe, kumburuza mahakamani pamoja na bodi ya sukari

Spread the loveMbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina (CCM) amesema amenuia kumpeleka mahakamani...

Biashara

Cheza sloti za Expanse kasino! mamilioni yanakusubiri 

Spread the love  Leo ni zamu yako kushinda na kuibuka Mfalme wa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Majahazi yadakwa na madumu 1,731 ya mafuta ya kupikia

Spread the loveKikosi kazi cha Polisi Wanamaji Dar es Salaam kimekamata majahazi...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa wa mauaji ya mtoto mwenye ualbino wafikishwa mahakamani

Spread the loveWATUHUMIWA wa mauaji ya Asimwe Novath, mtoto mwenye ualbino, wamefikishwa...

error: Content is protected !!