Sunday , 30 June 2024
Home Kitengo Michezo Serikali yaondoa kodi vifaa vya ‘VAR’
Michezo

Serikali yaondoa kodi vifaa vya ‘VAR’

Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania kupitia Waziri wa Fedha Dk. Mwigulu Nchemba wameondoa kodi kwenye vifaa vya teknolojia ya usaidizi wa refarii kwa njia ya video (VAR) Katika mwaka wa fedha wa 2024/25. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Mwigulu ameyasema hayo wakati akiwasilisha bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2024/25 leo tarehe 13 Juni 2024 Bungeni jijini Dodoma.

Katika hotuba yake Mwigulu alisema kuwa msimu ujao wa mashindano wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2024/25, kumepangwa kutumia teknolojia hiyo katika michezo ya Ligi Kuu ili kuepesha sintofahamau na maamuzi ya utata.

Kwenye kutekeleza hilo kupitia makadilio ya bajeti hiyo, Mwigulu alisema kuwa msimu ujao Ligi Kuu itaanza matumizi ya VAR ili kuhakikisha maamuzi yanakuwa ya haki

“Spika, napenda kulifahamisha Bunge lako Tukufu kuwa, msimu ujao wa Ligi Kuu ya Tanzania tutaanza kutumia ”VAR” ili kuhakikisha matokeo yanayopatikana uwanjani yanakuwa ya haki maana kuna timu zimezidi – msimu mmoja penati 10, halafu zikifungwa zenyewe magoli yanakataliwa.”

“Na ili tuwe na ”VAR” za kutosha katika viwanja vyote, naleta pendekezo la kutoa msamaha kwenye uingizaji wa mashine za ”VAR” na vifaa vyake kwa ufafanuzi utakaotolewa hapo baadae. INAWEZEKANA!” alisema Mwigulu

Wakati Mwigulu akiwasilisha nchi za Tanzania, Kenya na Uganda kwa sasa zipo kwenye maandalizi ya kuwa wenyeji wa michuano ya kombe la Mataifa Afrika (AFCON) 2027.

Katika Bajeti hiyo Serikali imepanga kukusanya na kutumia kiasi cha Shilingi 49.35 trilioni katika mwaka wa fedha wa 2024/25.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Leo ndiyo leo ukibashiri na Meridianbet

Spread the love Huna haja ya kujiuliza kuwa utapiga wapi mpunga siku...

Michezo

Anza wiki yako na mechi za EURO na Copa America Meridianbet

Spread the love  Jumatatu ya kupiga mkwanja na Meridianbet imefika rasmi ambapo...

Michezo

Ukiwa na Meridianbet ni kula pesa tu

Spread the love  Alhamisi ya leo mechi za EURO zinazidi kuendelea huku...

Michezo

Leo pesa utaipatia kwa Ureno na Uturuki ukiwa na Meridianbet

Spread the love  Kama kawaida michuano ya EURO 2024 inazidi kupamba moto...

error: Content is protected !!