Friday , 28 June 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali yaahidi kushirikiana na Prof. Ndakidemi kuhamasisha zao la kahawa
Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali yaahidi kushirikiana na Prof. Ndakidemi kuhamasisha zao la kahawa

Profesa Patrick Ndakidemi
Spread the love

Serikali imeahidi kuungana na Mbunge wa Moshi Vijijini, Profesa Patrick Ndakidemi (CCM), wakulima kutumia njia mbadala ya matumizi ya madawa kwenye uzalishaji wa kahawa ikiwa pamoja na kupanda miche chotara ambayo inazalishwa na kusambazwa bure na Bodi ya Kahawa Tanzania kwa kushirikiana na Taasisi ya Utafiti wa Kahawa Tanzania (TaCRI). Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Pia imetoa wito kwa wazalishaji viuatilifu vya asili kujisili kwa sababu serikali imepanga kununua zaidi ya lita 20,000 katika mwaka ujao wa fedha.

Hayo yamebainishwa leo Ijumaa bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Kilimo, David Silinde alipokuwa anajibu swali la Prof. Ndakidemi.

Katika swali la msingi Prof. Ndakidemi alihoji ni lini Serikali itarejesha utoaji wa ruzuku ya pembejeo za dawa kwa Wakulima wa Kahawa. Kwenye maswali ya nyongeza alihoji lini serikali itafanyia ukarabati mifereji ikiwamo Makeresho uliopo Kata ya Kibosho Magharibi wilayani Moshi vijijini ili kuwezesha wakulima kpata maji ya uhakika kumwagilia kahawa.

Akijibu maswali hayo, Silinde amesema tayari mfereji huo ipo kwenye mipango ya bajeti ya wizara hiyo na sasa inamtafuta mkandarasi.

Aidha, amesema miche ambayo inazalishwa na kusambazwa kwa wakulima ina ukinzani na magojwa makuu ya kahawa ya chole buni na kutu ya majani ambayo ndiyo yaliyokuwa yanasababisha mahitaji ya matumizi makubwa ya madawa.

“Katika msimu wa 2023/2024, jumla ya miche 21,899,560 ilizalishwa na kusambazwa kwa wakulima wa kahawa katika mikoa yote inayozalisha kahawa nchini. Kati ya miche hiyo, mkoa wa Kilimanjaro ulipata miche 1,664,635 ambayo imesambazwa kwa wakulima ambapo, Wilaya ya Moshi imepata jumla ya miche 328,110 na kusambazwa kwa wakulima kupitia Vyama vya Ushirika,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Dk. Mwinyi aipa tano Oryx kwa ujenzi wa bohari ya kuhifadhia gesi Znz

Spread the loveRAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk....

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Watanzania waonywa kutotumia uchaguzi kuvuna hela

Spread the loveWATANZANIA wametakiwa kutotumia uchaguzi kuwa wakati wa mavuno ya pesa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

MNEC CCM Rukwa atofautiana na Serikali kufungwa uvuvi Ziwa Tanganyika

Spread the loveWakati Serikali ikiwa imefunga shughuli za uvuvi katika Ziwa Tanganyika...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Taifa gesi yaja na mitungi ya bei nafuu kwa wanafunzi vyuo vikuu

Spread the loveKampuni ya kuuza nishati ya gesi ya kupikia majumbani ya...

error: Content is protected !!