Rais wa Kenya, William Ruto amekataa kutia saini Muswada wa Fedha wa 2024 kuwa sheria na kupendekeza marekebisho kadhaa kwenye muswada huo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).
Vyombo mbalimbali vya habari kutoka nchini humo vimeripoti kwamba Muswada huo utarejeshwa Bungeni kabla ya mapumziko leo Jumatano.
Bunge linaweza kurekebisha Muswada huo kwa kuzingatia mapendekezo ya rais au kuupitisha mara ya pili bila kuufanyia marekebisho.
Katika kurejesha muswada huo, rais ataonyesha maeneo muhimu ambayo yanahitaji kubadilishwa.
Hatua hiyo ni lazima, iwe imeungwa mkono na theluthi mbili ya wanachama.
Hayo yanajiri wakati wabunge hao wakitarajiwa kwenda mapumzikoni kuanzia leo hadi tarehe 23 Julai. Hata hivyo Spika wa Bunge hilo la Kenya atalazimika kuwarejesha wabunge hao ili kukamilisha marekebisho ya muswada.
Baadhi ya mapendekezo ya kodi ambayo awali yaliletwa katika muswada huo ni pamoja na asilimia 16 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani ya mkate, Ushuru wa Bidhaa kwenye mafuta ya mboga, VAT kwenye usafirishaji wa sukari, asilimia 2.5 ya Ushuru wa Magari na Ushuru wa mazingira kwa bidhaa zinazotengenezwa nchini.
Muswada huo ulipitishwa na kamati ya bunge zima baada ya marekebisho ya sasa kufanywa.
Muundo wa Kamati ya bunge zima inaruhusu uchunguzi wa kina wa kila kifungu, kuhakikisha uzingatiaji wa kina kabla ya muswada huo kuendelea hadi hatua zinazofuata za mapitio ya sheria.
Leave a comment