Friday , 28 June 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mazingira magumu ya JPM yamechangia ‘Comedy Journalism’
Habari za SiasaTangulizi

Mazingira magumu ya JPM yamechangia ‘Comedy Journalism’

Hayati Rais John Magufuli
Spread the love

Mwenyekiti wa Kamati ya kufuatilia hali ya uchumi wa vyombo vya Habari, Tido Mhando amesema kutokana na mazingira magumu ya kisheria na kisiasa ambayo vyombo vya habari vimepitia katika Serikali ya awamu ya Tano iliyokuwa chini ya Rais John Magufuli, vyombo vingi vya habari vimejidhibiti kutoa habari za uwajibikaji kwa umma na kuhamia maudhui mepesi ya mzaha ‘comedy journalism.’ Anaripoti Faki Ubwa …(endelea).

Pia amesema vyombo hivyo sasa vimebeba  maudhui ya burudani, mapenzi, muziki, michezo,  tamthilia na vipindi vyenye tija ndogo kwa jamii.

Mhando ameeleza hayo leo Jumanne wakati akiwasilisha mapendekezo ya kamati yake kwa Rais Samia Suluhu Hassan ambaye ni mgeni rasmi kwenye kongamano la maendeleo ya sekta ya habari.

Mhando amesema aina hiyo ya uandishi  inaleta madhara mawili makubwa, kwanza kudhoofisha uandishi unaozongatia uwajibikaji wa umma ambao ni muhimu kwenye jamii lakini pia kutengeneza kizazi kisochoweza kufikiria sawasawa kwa kuwa kinadumazwa na maudhui mepesi.

“Bila shaka sasa hivi tunaelewa kinachoendelea kuna kitu kinaitwa Comedy Journalism kumekuwa na mambo mengi ya mzaha mzaha yote haya yanatokana na wasiwasi waliokuwa nao waandishi, wamekuwa wanaogopa kutokana na mazingira magumu yaliyoletwa hapo mwanzo.

“Tunashukuru kwenye awamu yako hii ya sita yameanza kuondoka kidogo kidogo lakini kama ulivyotoa neno kwa viongozi hawa wa kisiasa wamekuwa wakileta ubabe ubabe katika sekta hii ya habari.

“Ubabe umekuwa mwingi tunaomba utasaidie kukabiliana na suala hili. Nina hakika hakuna chombo cha habari ambacho hakijatikiswa na ubabe huu kutoka kwa baadhi ya viongozi  mifano ni mingi lakini nisingependa kuitaja hapa kwa sababu ya muda,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Dk. Mwinyi aipa tano Oryx kwa ujenzi wa bohari ya kuhifadhia gesi Znz

Spread the loveRAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk....

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Watanzania waonywa kutotumia uchaguzi kuvuna hela

Spread the loveWATANZANIA wametakiwa kutotumia uchaguzi kuwa wakati wa mavuno ya pesa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

MNEC CCM Rukwa atofautiana na Serikali kufungwa uvuvi Ziwa Tanganyika

Spread the loveWakati Serikali ikiwa imefunga shughuli za uvuvi katika Ziwa Tanganyika...

Habari za SiasaKimataifa

Kenya waliamsha tena, maandamano yaanza kuelekea ikulu

Spread the loveWakenya kutoka maeneo ya Kisumu, Kisii, Mombasa na sehemu nyingine...

error: Content is protected !!