Tuesday , 2 July 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mahakama Kenya yaruhusu Jeshi kutumika kuzuia maandamano
Habari za SiasaKimataifa

Mahakama Kenya yaruhusu Jeshi kutumika kuzuia maandamano

Spread the love

Mahakama kuu nchini Kenya imeruhusu jeshi la nchi hiyo KDF kutumiwa katika kuwasaidia polisi kupambana na maandamano ya kupiga mswada wa fedha. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Hata hivyo, serikali imepewa siku mbili kutoa mwongozo wa kipindi na sehemu ambako jeshi litatumika katika kurejesha hali ya utulivu baada ya maandamano ya Jumanne na jana Alhamisi.

Katika uamuzi wake siku ya jana Alhamisi, Jaji Lawrence Mugambi alisema wanajeshi wamefunzwa kutumia nguvu, sio kutangamana na raia.

Wakati wa kusikilizwa kwa kesi iliyowasilishwa na Chama cha Mawakili nchini Kenya (LSA), Jaji aliuliza maswali kadhaa kwa pande zote zilizokuwepo huku akitaka kuelewa vipengele vya operesheni za kijeshi na sheria mahususi kwa vikosi vya ulinzi.

Aliitaka LSK kutoa maoni kuhusu matukio ambayo KDF inaweza kutumwa ambapo chama hicho ilitaja kifungu cha 241 cha katiba.

Kwa upande wake, serikali inatetea hatua yake ikisema hakuna chochote kinachokiuka sheria katika notisi ya gazeti la serikali iliyotolewa na Waziri wa Ulinzi Aden Duale.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoKimataifa

Tofauti kati ya Rais Ruto, Naibu wake zaanikwa

Spread the loveTOFAUTI za kimtizamo kati ya Rais William Ruto na Naibu...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Maandamano yaibuka upya Kenya

Spread the loveVIJANA wa Kenya waliojipachika jina la Generation Z (Gen Z)...

BiasharaHabari MchanganyikoHabari za Siasa

TRA yaweka rekodi makusanyo 2024, yakusanya trilioni 27.64

Spread the loveWAKATI wafanyabiashara nchini wakiweka mgomo wa siku tatu kupinga makadirio...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CAG atoa kongole kwa PPAA

Spread the loveMDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles...

error: Content is protected !!