Sunday , 30 June 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Mwigulu: Rais Samia amekopa trilioni 17.2
Habari za SiasaTangulizi

Dk. Mwigulu: Rais Samia amekopa trilioni 17.2

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

Waziri wa Fedha, Dk. Mwigulu Nchemba amesema katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Sita, wamekopa jumla ya Sh 17.2 trilioni kutoka katika vyanzo vya nje kwa lengo la kugharamia shughuli mbalimbali za maendeleo.

Amesema fedha hizo zimeelekezwa kwenye miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo: Mradi wa Ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) kwa vipande mbalimbali pamoja na ununuzi wa mabehewa na vichwa  vya  treni.

Akiwasilisha bungeni jijini Dodoma leo Alhamisi mapendekezo ya serikali kuhusu makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2024/2025, amesema mikoa itakayonufaika na mradi huu ni pamoja na Dar es Salaam, Morogoro, Dodoma, Singida, Tabora, Shinyanga, Mwanza, Katavi na Kigoma.

“Miradi hii pia itafungua fursa za kiuchumi kutoka nchi  jirani kama vile Burundi  na  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Mpina amng’ang’ania Bashe, kumburuza mahakamani pamoja na bodi ya sukari

Spread the loveMbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina (CCM) amesema amenuia kumpeleka mahakamani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Majahazi yadakwa na madumu 1,731 ya mafuta ya kupikia

Spread the loveKikosi kazi cha Polisi Wanamaji Dar es Salaam kimekamata majahazi...

Habari za SiasaKimataifa

30 wafariki dunia maandamano Kenya

Spread the loveShirika la Human Rights Watch limesema takriban watu 30 walifariki...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Tanzania yakubali kukutana na mabalozi 9 kutatua changamoto za kikodi

Spread the loveSerikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na...

error: Content is protected !!