Mhandisi Mkama Bwire ameteuliwa kushika nafasi ya Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar Es Salaam (DAWASA) katika kikao maalum cha Waziri wa Maji na Bodi ya Wakurugenzi DAWASA kilichofanyika leo tarehe 3 Julai, 2024 ofisi za DAWASA Dar Es Salaam.
Taarifa iliyotolewa na Idara ya Mawasiliano DAWASA imesema Mhandisi Bwire ni Mtumishi wa Wizara ya Maji ambaye amehudumu kama Mhandisi wa Maji katika Halmashauri ya Kibaha.
Pia amewahi kuhudumu katika nafasi ya Mkurugenzi Mtendaji Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Tabora (TUWASA).
na hadi anapokea jukumu hilo alikua ni Mkurugenzi wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini katika Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA).
Bwire amechukua nafari ya Kiunga Kingu ambaye alisimamishwa na Waziri wa Maji, Jumaa Aweso kutokana na malalamiko ya wananchi kuhusu uhaba wa maji Dar es Salaam.
Aweso pia alimsimamisha kazi, Mkurugenzi wa Uzalishaji na Usambazaji Maji-DAWASA, Shaban Mkwanywe na kuiweka DAWASA chini ya uangalizi Wizara ili kuboresha utendaji wake kufuatia uzembe uliopelekea visima kukosa maji na kufanya Wakazi wa Dar es salaam kukosa maji.
Leave a comment