Sunday , 30 June 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bilioni 155.4 kugharamia kicheko cha wastaafu 2022-2030
Habari za SiasaTangulizi

Bilioni 155.4 kugharamia kicheko cha wastaafu 2022-2030

Wastaafu
Spread the love

Waziri wa Fedha, Dk. Mwigulu Nchemba amesema jumla ya Sh 155.4 bilioni zinatarajiwa kupungua kwenye mapato ya Serikali kutokana na pendekezo la kufanya maamuzi ya muda mfupi ya kugharamia malipo ya nyongeza ya mkupuo kwa watumishi wa umma waliostaafu kuanzia mwaka 2022/2023 na watakaostaafu kuendelea hadi 2029/2030. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Amependekeza malipo ya mkupuo kwa wastaafu kwa asilimia saba ili kufikia asilimia 40 kwa kundi ambalo lilikuwa linalipwa asilimia 50  kabla  ya kuunganishwa kwa mifuko ya pensheni.

Pia amependekeza kuongeza kikokotoo kwa asilimia mbili ili kufikia asilimia 35 kwa kundi ambalo lilikuwa linalipwa asilimia 25 kabla ya kuunganishwa kwa mifuko ya pensheni.

Akiwasilisha bungeni jijini Dodoma leo Alhamisi kuhusu makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2024/2025, amesema nyongeza hizo zitaanza kulipwa kwa wastaafu waliostaafu kuanzia mwaka 2022/23 na kuendelea hadi watakaostaafu mwaka 2029/30 na baada ya hapo mfuko wa  PSSSF  uchukue jukumu la kuendelea kuwalipa mafao.

“Lengo la hatua hii ni kutoathiri mfumo mzima wa pensheni kwa kuwa na uwiano wa mafao kwa wanachama na kuupa Mfuko muda wa kuangalia uhimilivu wake. Hatua hii inatarajiwa kupunguza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 155,400,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Mpina amng’ang’ania Bashe, kumburuza mahakamani pamoja na bodi ya sukari

Spread the loveMbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina (CCM) amesema amenuia kumpeleka mahakamani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Majahazi yadakwa na madumu 1,731 ya mafuta ya kupikia

Spread the loveKikosi kazi cha Polisi Wanamaji Dar es Salaam kimekamata majahazi...

Habari za SiasaKimataifa

30 wafariki dunia maandamano Kenya

Spread the loveShirika la Human Rights Watch limesema takriban watu 30 walifariki...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Tanzania yakubali kukutana na mabalozi 9 kutatua changamoto za kikodi

Spread the loveSerikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na...

error: Content is protected !!