Sunday , 30 June 2024
Home Kitengo Biashara Bei mafuta ya petroli, dizeli zashuka
BiasharaHabari MchanganyikoTangulizi

Bei mafuta ya petroli, dizeli zashuka

Spread the love

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), imetangaza bei kikomo ya mafuta ya petroli kupitia Bandari ya Dar es Salaam inayoanza kutumika leo tarehe 5 Juni 2024, kuwa imeshuka kwa Sh52.72 na kufikia Sh3, 261 kwa lita moja, ikilinganishwa na bei ya mwezi uliopita. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Taarifa iliyotolewa Ewura leo Jumatano imeonyesha bei ya dizeli inayochukuliwa kwenye bandari hiyo ya Dar es Salaam pia imeshuka hadi Sh3,112 kutoka Sh3,196 iliyokuwa inatumika mwezi uliopita.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa kupungua huko kumetokana na kupungua kwa bei ya mafuta yaliyosafishwa katika soko la dunia (FBO) kwa wastani wa asilimia 11.82 kwa petroli na asilimia 7.77 kwa dizeli na asilimia 7.94 kwa mafuta ya taa.

“Pia kuongezeka kwa wastani wa gharama za kubadilisha fedha za kigeni (Applicable Exchange Rate) kwa 1.4%; kupungua kwa gharama za uagizaji wa mafuta (premiums) kwa wastani wa asilimia 2.06 kwa petroli na asilimia 8.51 kwa dizeli katika Bandari ya Dar es Salaam;

“Kuongezeka kwa gharama za uagizaji wa mafuta kwa wastani wa asilimia 7.07 kwa petroli na asilimia 25.24 kwa dizeli katika Bandari ya Tanga; na kupungua kwa wastani wa asilimia 12.64 kwa mafuta ya petroli na 12.61 kwa mafuta ya dizeli katika Bandari ya Mtwara,” imesema taarifa hiyo iliyosainiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Ewura, Dk James Mwainyekule.

Dk James Mwainyekule.

Aidha, kwa Bandari ya Tanga bei ya petroli imeshuka hadi Sh3,263 kutoka Sh 3,360 kwa mwezi uliopita kwa upande wa dizeli nayo imeshuka hadi Sh 3,121 kutoka Sh 3,242.

Katika Bandari ya Mtwara petroli imeshuka na itauzwa kwa rejareja kwa Sh 3,267 kutoka Sh 3,317 kwa mwezi uliopita na dizeli itauzwa Sh3,122 kutoka Sh3,200 mwezi uliopita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Mpina amng’ang’ania Bashe, kumburuza mahakamani pamoja na bodi ya sukari

Spread the loveMbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina (CCM) amesema amenuia kumpeleka mahakamani...

Biashara

Cheza sloti za Expanse kasino! mamilioni yanakusubiri 

Spread the love  Leo ni zamu yako kushinda na kuibuka Mfalme wa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Majahazi yadakwa na madumu 1,731 ya mafuta ya kupikia

Spread the loveKikosi kazi cha Polisi Wanamaji Dar es Salaam kimekamata majahazi...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa wa mauaji ya mtoto mwenye ualbino wafikishwa mahakamani

Spread the loveWATUHUMIWA wa mauaji ya Asimwe Novath, mtoto mwenye ualbino, wamefikishwa...

error: Content is protected !!