Friday , 5 July 2024
Home Habari Mchanganyiko Manji afariki dunia, Yanga wamlilia
Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Manji afariki dunia, Yanga wamlilia

Spread the love

MFANYABIASHARA maarufu nchini, Yusuf Manji amefarikia dunia leo Jumapili jijini Florida nchini Marekani baada ya kuugua kwa muda mfupi. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Uongozi wa Young Africans Sports Club umethibitisha kifo cha Manji ambaye alikuwa mfadhili wa timu hiyo kuanzia 2012 hadi 2017 Mei alipojiuzulu.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Klabu ya Yanga imesema imepokea hiyo kwa mshtuko na masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Manji aliyewahi kuwa Mdhamini na Mwenyekiti wa Klabu.


“Kifo cha Marehemu Manji kimetokea leo, Juni 30. 2024, nchini Marekani alipokuwa akipatiwa matibabu “ imesema taarifa hiyo.

Rais wa Young Africans Sports Club, Eng Hersi Said amesema enzi za uhai wake, Yusuf Manji alikuwa kiongozi mahiri aliyejituma na kujitoa kwa ajili ya kuijenga KIabu ya Yanga.

“Hi ni pigo kubwa kwetu Young Africans Sports Club na familia ya michezo kwa ujumla. Tutamkumbuka Yusuf Manji kwa mapanzi yake makubwa aliyokuwa nayo kwa Klabu yetu na namna alivyokuwa akijitoa kwa hali na mali katika kuiendeleza sekta ya michezo Tanzania,” amesema Rais Eng, Hersi Said.

Manji alihudumu katika nafasi mbalimbali za kiuongozi ndani ya Klabu ya Yanga  kama Mdhamini na Mwenyekiti ambapo hadi umauti unamkuta alikuwa Mwanachama wa Young Africans Sports club.

“Uongozi wa Young Africans Sports Club, unatoa pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki na wanamichezo wote nchini kwa msiba mzito wa mpendwa wetu.

“Tunamuombea kwa Mwenyezi Mungu aipumzishe pho ya Marehemu mahala pema Peponi, Amina. Sisi ni wa Mwenyezi Mungu na kwake tutarejea,” amesema.

1 Comment

  • Poleni sana familia ya marehemu Yusuf Manji na Yanga. Ninaomba masahihisho hapa. Florida siyo jiji, ni jimbo. Sasa, jiji au mji unaitwaje?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

TCB yaja na huduma za ubunifu kidijitali maonesho Sabasaba

Spread the loveBenki ya Biashara Tanzania (TCB) ambayo ni moja ya taasisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Kampuni ya DL GROUP kulipa wafanyakazi ndani siku saba

Spread the loveMWEKEZAJI wa viwanda na mashamba ya chai yaliyopo mkoani Iringa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Shilole balozi mpya Oryx gesi kuhamasisha matumizi nishati safi

Spread the loveKAMPUNI ya Gesi ya Oryx imemtangaza Mama Lishe, Zuwena Mohamed...

ElimuHabari Mchanganyiko

NMB yazipiga tafu sekondari Dar kwa vifaa vya milioni 10

Spread the loveBenki ya NMB imekabidhi meza 90 na viti 90 vyenye...

error: Content is protected !!