Thursday , 4 July 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mahakama Kenya yaruhusu Jeshi kutumika kuzuia maandamano
Habari za SiasaKimataifa

Mahakama Kenya yaruhusu Jeshi kutumika kuzuia maandamano

Spread the love

Mahakama kuu nchini Kenya imeruhusu jeshi la nchi hiyo KDF kutumiwa katika kuwasaidia polisi kupambana na maandamano ya kupiga mswada wa fedha. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Hata hivyo, serikali imepewa siku mbili kutoa mwongozo wa kipindi na sehemu ambako jeshi litatumika katika kurejesha hali ya utulivu baada ya maandamano ya Jumanne na jana Alhamisi.

Katika uamuzi wake siku ya jana Alhamisi, Jaji Lawrence Mugambi alisema wanajeshi wamefunzwa kutumia nguvu, sio kutangamana na raia.

Wakati wa kusikilizwa kwa kesi iliyowasilishwa na Chama cha Mawakili nchini Kenya (LSA), Jaji aliuliza maswali kadhaa kwa pande zote zilizokuwepo huku akitaka kuelewa vipengele vya operesheni za kijeshi na sheria mahususi kwa vikosi vya ulinzi.

Aliitaka LSK kutoa maoni kuhusu matukio ambayo KDF inaweza kutumwa ambapo chama hicho ilitaja kifungu cha 241 cha katiba.

Kwa upande wake, serikali inatetea hatua yake ikisema hakuna chochote kinachokiuka sheria katika notisi ya gazeti la serikali iliyotolewa na Waziri wa Ulinzi Aden Duale.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko awataka Watanzania kulinda viumbe hai baharini

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaKimataifa

Waingereza kuifuta historia ya Conservatives leo?

Spread the loveWaingereza milioni 50 wanatarajiwa kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu leo...

Habari za SiasaKimataifa

Rais Biden agoma kujitoa uchaguzi Novemba, aangukia pua kura za maoni

Spread the loveRAIS wa Marekani, Joe Biden amekataa kujitoa kwenye uchaguzi wa...

BiasharaHabari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia, Nyusi wapongeza mkakati wa utanuzi PBZ, yakaribishwa kufungua tawi Msumbiji

Spread the loveRais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amepongeza jitihada zinazofanywa na...

error: Content is protected !!