Thursday , 4 July 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Waandamanaji wavamia Bunge, wabunge watimua mbio, 8 wafariki dunia
Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Waandamanaji wavamia Bunge, wabunge watimua mbio, 8 wafariki dunia

Spread the love

WABUNGE wa Bunge la Kenya wamelazimika kukimbia ofisi zao zilizoko Bunge Towers baada ya waandamanaji wanaopinga ushuru kwenye Muswada wa Fedha 2024, kuvamia majengo ya Bunge la nchi hiyo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa… (endelea).

Hata hivyo, tayari muswada huo unaolenga kuiwezesha Serikali ya Kenya kukusanya Ksh 347 bilioni (Sh trilioni saba), umepitishwa na baada ya wabunge 195 kupiga kura ya NDIO kuunga mkono muswada huo ulivyofanyiwa marekebisho huku wabunge 106 wakiupinga.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka vyanzo mbalimbali nchini Kenya, imeeleza waandamanaji nane wanadaiwa kupoteza maisha baada ya polisi kutumia risasi kuwasambaratisha waandamanaji hao.

Waandamanaji hao waliojawa na hamaki walivunja geti la uani la Bunge kupitia upande wa Uhuru Highway, kisha kuingia ndani na kuvunja vyoo na kufanya uharibifu pamoja na kula vyakula vya wabunge.

Maafisa wa polisi ambao wengi wao walionekana kulemewa na wingi wa waandamanaji hao walibaki kuwaangalia wasijue la kufanya huku vijana wakiingia kila upande mithili ya nyuki.

Waandamanaji hao waliingia ndani ya Bunge saa chache baada ya polisi kuwapiga risasi waandamanaji kadhaa nje ya Majengo ya Bunge.

Waandamanaji hao pia walichoma magari ya Polisi huku hali ya wasiwasi ikiongezeka nje ya bunge.

Hii ni mara ya kwanza katika historia ya Kenya kwa waandamanaji kuvunja vizuizi na kuingia ndani ya Bunge licha ya ulinzi mkali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko awataka Watanzania kulinda viumbe hai baharini

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaKimataifa

Waingereza kuifuta historia ya Conservatives leo?

Spread the loveWaingereza milioni 50 wanatarajiwa kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu leo...

Habari za SiasaKimataifa

Rais Biden agoma kujitoa uchaguzi Novemba, aangukia pua kura za maoni

Spread the loveRAIS wa Marekani, Joe Biden amekataa kujitoa kwenye uchaguzi wa...

BiasharaHabari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia, Nyusi wapongeza mkakati wa utanuzi PBZ, yakaribishwa kufungua tawi Msumbiji

Spread the loveRais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amepongeza jitihada zinazofanywa na...

error: Content is protected !!