Friday , 17 May 2024
Home Habari Mchanganyiko NMB wagawa zaidi ya mil. 24 kwa washindi Mastabata
Habari Mchanganyiko

NMB wagawa zaidi ya mil. 24 kwa washindi Mastabata

Spread the love

WASHINDI 120 wa kampeni ya Benki ya NMB ya mastabata- halipoi wamejinyakulia jumla ya zaidi ya Sh milioni 24 kama zawadi katika droo yake ya pili ya mwisho wa mwezi wa Disemba 2023 ya kampeni hiyo inayolenga kuhamasisha matumizi ya kadi na kulipa kwa kuskani QR katika kufanya malipo.  Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

 NMB imegawa zawadi hizo tarehe 29 Disemba 2023 kwenye droo maalum iliyochezeshwa jijini Arusha, ambapo pia washindi watatu wamefanikiwa kushinda safari ya Kendwa rocks na wenza wao huko Zanzibar watakaogharamiwa usafiri, malazi na chakula pia posho ya Sh 200,000. 

 Droo hiyo ilitoa washindi 100 wa kila wiki waliojishindia kila mmoja shilingi 100,000 na wateja 17 wa mwezi waliojishindia kila mmoja Sh 500,000 taslimu.

 Akizungumzia droo hiyo, wakati wa ugawaji wa zawadi, meneja mwandamizi wa NMB idara ya Biashara ya kadi Manfredy Kayala amesema washindi hao 120 ni wa mwezi huu ambapo wamegawiwa jumla ya Sh 24.5 ikiwemo milioni 10 za washindi 100 wa kila wiki ambapo kila mmoja alijishindia Sh 100,00. 

 “Mbali na hao, washindi 17 wa mwezi wamejishindia shilingi 500,000 kila mmoja, huku washindi watatu wakipata safari ya kugharamiwa kwenda Zanzibar na wenza wao na watapewa posho ya 200,000,” alisema Kayala. 

 Kayala alisema zawadi hizo ni sehemu ya zawadi ya Sh milioni 350 walizotenga kutoa kama zawadi zikiwa ni pesa taslimu pamoja na safari za kwenda kupumzika katika visiwa vya Zanzibar na nchini Afrika Kusini. 

 “Kwa kampeni hii ya awamu ya tano, kuna zaidi ya washindi 1200 wa kila wiki wanaopata 100,000/- katika kampeni zinazoendelea pamoja na washindi 240 wa papo hapo ambao wanapata 50,000/- wanapofungua akaunti au kujibu maswali kadhaa. Hiyo ni pamoja na washindi wa kila mwezi ambao kila mmoja atapata 500,000,”  alisema. 

 Alisema kampeni hiyo inalenga kuhamasisha matumizi yasiyotumia fedha taslim na badala yake watumie kadi, kuskani QR au malipo ya kiktandao ambayo itapunguza kiwango cha uhalifu unaohusisha watu kuibiwa fedha zao kama ilivyokuwa zamani lakini pia kukuza uchumi.  

Kaimu Meneja wa NMB Kanda ya Kaskazini, Praygod Godwin alieleza kuwa promosheni hiyo maalum inatekelezwa na benki hiyo kwa kushirikiana na kitengo Mastercard. 

 Alisema Benki hiyo yenye matawi zaidi ya 43 Kanda ya kaskazini, itaendeleabkujanna promosheni mbalimbali ili kuendelea kuwanufaisha wateja wanaotunia huduma za Benki hiyo. 

 “Ukiwa na Kadi ya NMB mtu anaweza kufanya miamala wakati wowote na mahali popote ambapo kuna Pointi za Mauzo (POS),” alisema 

 Mmoja wa wateja walioshinda droo hiyo, mfanyabiashara Jackline Matowo, alisema alienda benki kuweka pesa kwa ajili ya biashara yake lakini akabahatika kucheza droo ya papo hapo na kushinda Sh 50,000/- katika kampeni inayoendelea. 

 “NMB wamefanya kampeni nzuri haswa ambayo inahamasisha wateja kuendelea kutumia huduma za kifedha kidigitali kwa kutambua zawadi hizi lakini inaleta usalama wa fedha zetu na zaidi inasaidia nchi kujua maendeleo yake kiuchumi” alisema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Nape aomba bajeti ‘kiduchu’ kwa mwaka 2024/25

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Seneta: Wanasiasa hawasaidii mchakato wa Katiba mpya

Spread the loveSeneta wa jimbo la Busia, nchini Kenya, Okiya Okoiti Andrew...

Habari Mchanganyiko

Wananchi washauriwa kuongeza uelewa wa kujikinga na majanga

Spread the love WITO umetolewa kwa wananchi kuongeza uelewa na utayari kabla...

error: Content is protected !!