Saturday , 18 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Tanzania yapongezwa kurejesha amani DRC, ICGLR
Habari Mchanganyiko

Tanzania yapongezwa kurejesha amani DRC, ICGLR

Spread the love

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepongezwa kwa kuendelea kuwa mstari wa mbele kurejesha amani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Ukanda wa Maziwa Makuu. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Pongezi hizo zimetolewa Mjumbe Maalum wa Katibu Mkuu Umoja wa Mataifa katika Ukanda wa Maziwa Makuu, Balozi Huang Xia alipokutana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba – Jijini Dar es Salaam.

“Umoja wa Mataifa tunaipongeza Tanzania kwa kulinda misingi ya amani na kuwa mstari wa mbele katika kurejesha amani na usalama katika Ukanda wa Maziwa Makuu,” alisema Balozi Huang.

Huang ameongeza kuwa ni wakati muafaka kwa viongozi wa Ukanda wa Maziwa Makuu kusaidia kuhakikisha kuwa amani inapatikana Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ili kuliwezesha taifa hilo kusonga mbele kiuchumi na kisiasa.

Kwa upande wake Waziri Makamba ameupongeza Umoja wa Mataifa kwa kuendelea kudumisha amani katika ukanda wa Maziwa Makuu kwani ndiyo njia itakayosaidia kuwalinda raia na kukuza uchumi katika ukanda huo.

“Tanzania chini ya uongozi imara wa Rais, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, inaamini amani ndio msingi pekee wa maendeleo kwa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla,” alisema Waziri Makamba.

Pamoja na mambo mengine, Waziri Makamba amemhakikishia Balozi Huang kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana na Umoja wa Mataifa na Jumuiya za Kimataifa na za Kikanda kurejesha amani na usalama katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Ukanda wa Maziwa Makuu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yazindua bima ya afya kwa wakulima

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na kampuni...

Habari Mchanganyiko

Makamba awasili China kwa ziara ya kikazi

Spread the loveWaziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,...

Habari Mchanganyiko

Ethiopia yafungua njia ujenzi wa ubalozi Dodoma

Spread the loveSerikali ya Tanzania imeipongeza Serikali ya Ethiopia kwa kuweka historia...

error: Content is protected !!