Saturday , 18 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Haya hapa majina wafanyabiashara 13 waliofariki ajalini Songea
Habari Mchanganyiko

Haya hapa majina wafanyabiashara 13 waliofariki ajalini Songea

Spread the love

 

JESHI la Polisi wa Mkoa wa Ruvuma limetaja majina ya wafanyabiashara 13 waliofariki dunia katika ajali iliyotokea usiku wa kuamkia jana tarehe 10 Aprili 2023 baada ya gari aina ya Mitsubishi Fuso walilokuwa wakisafiria kutumbukia katika daraja la Mto Njoka Namatuhi lililopo barabara ya Ndongosi – Namatuhi, Songea vijijini. Anaripoti Mwandishi Wetu, Ruvuma … (endelea).

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, Marco Chilya amesema gari hilo lenye namba za usajili T800 BXB, lililokuwa likiendeshwa na Thobias Njovu, liliacha njia na kutumbukia mtoni mara baada ya kushindwa kupanda Mlima.

Aidha, Kamanda Chilya amewataja waliofariki kwenye ajali hiyo ambao wengine walifahamika kwa jina moja kuwa ni Happy Msemwa, Jafari Ngalimus, Hidaya Salum, Biesha Yahaya, Mustafa Ally, Mwaisha, Hamad, Juma Said, Boniface na Christofa Msuya.

Wengine ni Deograsia Mapunda, Simba na mama Faraja huku akiwataja majeruhi kuwa ni Hamis Mbawala na Christofa Banda na wamelazwa katika kituo cha afya cha Mpitimbi na kwamba miili ya marehemu imehifadhiwa katika Hospitali ya Mkoa wa Songea.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yazindua bima ya afya kwa wakulima

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na kampuni...

Habari Mchanganyiko

Makamba awasili China kwa ziara ya kikazi

Spread the loveWaziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,...

Habari Mchanganyiko

Ethiopia yafungua njia ujenzi wa ubalozi Dodoma

Spread the loveSerikali ya Tanzania imeipongeza Serikali ya Ethiopia kwa kuweka historia...

error: Content is protected !!