Friday , 17 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Watuhumiwa kesi 147 za rushwa waachiwa huru
Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa kesi 147 za rushwa waachiwa huru

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Utumishi, Jenista Mhagama
Spread the love

 

SERIKALI imesema watuhumiwa wa kesi 147 za rushwa wameachiwa huru baada ya kutopatikana na hatia katika kipindi cha mwaka mmoja. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Hayo yameelezwa leo Alhamisi tarehe 21 Aprili, 2022 bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Jenista Mhagama.

Amesema kesi hizo ni kati ya kesi 865 za tuhuma dhidi ya rushwa na ufisadi zilizoendeshwa mahakamani zikiwemo kesi mpya 305.

Amesema, kesi 338 ziliamuliwa mahakamani ambapo kesi 191 watuhumiwa walipatikana na hatia na kuhukumiwa kifungo au kulipa faini.

“Kesi 147 watuhumiwa wake hawakupatikana na hatia na kuachiwa huru. Kesi 527 bado zinaendelea mahakamani,” amesema Mhagama.

Katika hatua nyingine amesema Sh. bilioni 1.42 zimeokolewa kutokana na operesheni mbalimbali za uchunguzi uliofanyika kote nchini.

Amesema taasisi hiyo kwa kushirikiana na mamlaka nyingine imewezesha kutaifisha na kurejesha Serikalini fedha na mali zenye thamani ya Sh. bilioni 6.3 na dola za kimarekani 1,468,364 ambazo zinahusisha fedha, nyumba tano, viwanja sita na magari saba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Nape aomba bajeti ‘kiduchu’ kwa mwaka 2024/25

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Seneta: Wanasiasa hawasaidii mchakato wa Katiba mpya

Spread the loveSeneta wa jimbo la Busia, nchini Kenya, Okiya Okoiti Andrew...

Habari Mchanganyiko

Wananchi washauriwa kuongeza uelewa wa kujikinga na majanga

Spread the love WITO umetolewa kwa wananchi kuongeza uelewa na utayari kabla...

error: Content is protected !!