Sunday , 19 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Jaji Warioba: Dk. Mwele aniomba ushauri kugombea urais 2015
Habari Mchanganyiko

Jaji Warioba: Dk. Mwele aniomba ushauri kugombea urais 2015

Spread the love

 

WAZIRI Mkuu mstaafu, Jaji Joseph Warioba amesema Dk. Mwele Malecela kabla ya kuchukua fomu kuwania kupitishwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika kinyang’anyiro cha urais 2015, alimfuata nyumbani kwake kumuomba ushauri. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea). 

Jaji Warioba ametoa kauli hiyo wakati akizungumza katika ibada ya kuaga mwili wa Dk. Mwele iliyofanyika leo tarehe 19 Februari, 2022 katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.

Dk. Mwele (58) ambaye hadi umauti unamfika Tarehe 10 Februari, 2022, alikuwa Mkurugenzi wa Magonjwa yasiyopewa Kipaumbele katika Shirika la Afya Duniani (WHO).

Akimueleza Dk. Mwele, Jaji Warioba amesema alikuwa akipata taarifa za Dk. Mwele kutoka kwa mwanaye anayefahamika kwa jina la Jane ambaye walisoma wote shule ya Skondari Weruweru mkoani Kilimanjaro.

Dk. Mwele Malecela, Mkurugenzi wa Vituo vya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa Afrika vya Shirika la Afya Duniani (WHO)

“Mtu aliyekuwa akituambia hali yake ni Jane, alikuwa akiwasiliana naye na mara ya mwisho siku chache kabla ya kifo chake, alikuja kunieleza kuwa aliwasiliana na Dk. Mwele akawa na wasiwasi, ndipo akapata taarifa kuwa ametutuoka..

“Dk. Mwele alikuwa ni mtu anayejiamini, alijiamini sana, mwaka 2015 alikuja kwangu kutaka ushauri kama achukue fomu kugombea urais.

“Nikamwambia Mwele unaona una uzito wa kutosha kuingia katika kundi hili? akaniambia baba ( Mzee Samuel Malecela) naye amesema hivyohivyo, lakini mimi naamini naweza… kweli aliingia alikuwa ni mtu anajiamini hakuogopa kitu chochote.

Jaji,Joseph Warioba Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba

“Mwele ametuachia legacy lakini tumemuona kwa utumishi wake, lakini legacy kubwa tumemuona kama binadamu alivyokuwa akiwalea wengine.

“Mwenyezi Mungu ameona ni wakati wake amchukue Dk. Mwele na tushukuru kwa maisha aliyompa hadi kufikia sasa,” amesema Jaji Warioba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Canada yatenga bilioni 38 kutekeleza mradi ya kuinua vijana TZ

Spread the loveSERIKALI ya Canada kupitia ‘CARE International Canada’ imetenga takribani Sh...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari Mchanganyiko

Balile ateuliwa rais wa wahariri Afrika Mashariki

Spread the loveJumuiya ya Wahariri wa Afrika Mashariki (EAES), imemchagua Mwenyekiti wa...

error: Content is protected !!