MBUNGE wa Jimbo la Kigoma Mjini Zitto Kabwe ameipongeza Serikali kwa kuifanya Kigoma kuwa bandari ya mwisho kwa mizigo inayokwenda Kongo na Burundi, anaadika Mwandishi Wetu.
Kabwe alitoa pongezi hizo wakati akizungumza na Mawaziri wa Tanzania, Kongo, Burundi, Zambia na Uganda katika ukumbi wa Lake Tanganyika jana.
Alisema hivyo uchumi wa Kigoma utaongezeka kwa kiasi kikubwa kwa sababu Burundi peke yake inaagiza mizigo kupitia bandari ya Dar es salaam zaidi ya tani 350, 000.
“Mimi napenda niipongeze sana serikali yetu kwa kuweza kufanya kazi kwa pamoja na wenzetu wa nchi za jirani kama Burundi, Kongo, Zambia na Uganda kwa kuweza kukubaliana maazimio waliyokubaliana katika mkutano huu.
Jambo la msingi ambalo napenda kulisisitiza ni kuimarisha reli kwa sababu kama tunataka mzingo uweze kufika Bukavu kwa harakakupitia bandari ya Kigoma lazima reli ya kati ifanye kazi vizuri”alisema Zitto.
Alisema kama reli ikifanya kazi vizuri hapo ndipo uchumi wa Kigoma utakuwa sana kwa sababu mtu akisafirisha mizigo kutoka Dar es salaam kwa reli hadi Kigoma itakuwa ni raisi sana kuliko kuisafirisha kwa barabara.
Alisema serikali ikiimarisha reli ya kati mzunguko wa fedha katika mkoa wa kigoma utaongezeka sana na kufanya watu kujenga mahoteli, watazalisha chakula na kutumia fedha za hapa na hivyo kudumisha mkoa wa Kigoma.
“Kwa hiyo sisi ambao tumekulia hapa Kigoma ni jambo la historia pia nawapongeza Mawaziri wote ambao wameshiliki katika mkutano huu pamoja na serikali zote kufanya Kigoma kuwa lango kuu wa biashara.
Aidha Mawaziri waliyohudhulia mkutano huo ni Makame Mbarawa wa Tanzania, John Bosco wa Burundi, Aggrey Bagire wa Uganda, Niyonkuru Pelalte wa Burundi.
Leave a comment