Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbatia apinga kufungiwa, kuendelea na kampeni
Habari za Siasa

Mbatia apinga kufungiwa, kuendelea na kampeni

James Mbatia, Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi
Spread the love

JAMES Mbatia, Mgombea Ubunge wa Vunjo Mkoa wa Kilimanjaro kupitia NCCR-Mageuzi, ameupinga uamuzi uliotolewa na Kamati ya Maadili Jimbo hilo wa kumfungia kwa siku saba kutokufanya kampeni kuanzia leo Jumamosi tarehe 17 hadi 23 Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kilimanjaro … (endelea).

Uamuzi huo ulitolewa jana Ijumaa na kikao hicho, baada ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwasilisha malalamiko kwamba, Mbatia anatumia vipeperushi ambavyo havijasajiliwa na msimamizi wa uchaguzi.

Mkuu wa Idara ya Uenezi na Mahusiano ya Umma wa NCCR-Mageuzi, Edward Simbeye akizungumza na MwanaHALISI ONLINE amesema, “uamuzi huo ni batili, kikao kilichofanyika ni batili na tunaendelea na kampeni kama kawaida.”

Simbeye aliyeko jimboni kwa Mbatia amesema, vipeperushi vinavyozungumzwa vinaelezea mambo aliyoyafanya Mbatia kwa kipindi cha miaka mitano (2015-2020).

Amesema, kwa mujibu wa Maadili ya Uchaguzi kipengele cha 5:4 kinazungumzia, kama kuna maadili yamekiukwa, “kiwasilishe kwa msimamizi kwa njia ya maandishi, lakini CCM haijafanya hivyo, tuliomba kupewa hayo malalamiko yao kwa maandishi, hatukupewa.”

Edward Sembeye, Mkuu wa Mawasiliano ya Umma NCCR-Mageuzi

Simbeye amesema, baada ya Mbatia ambaye pia ni Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi kupewa malalamiko hayo, “aliyajibu lakini cha kushangaza, katika kikao cha jana utetezi wake aliouwasilisha kwa maandishi, haukusomwa, sasa unawezaje kuamua bila kusikiliza utetezi wa anayelalamikiwa.”

Pia, amesema, kikao kilichokaa jana, kilihusisha majimbo mawili jambo ambalo ni kinyume na taratibu za uchaguzi “yaani mgombea wetu, amehukumiwa na vikao viwili vya majimbo badala ya kimoja. Ndiyo maana tunasema ni batili na sisi tutaendelea na kampeni kama kawaida kesho.”

MwanaHALISI ONLINE linaendelea na jitihaza za kumtafuta msimamizi wa uchaguzi jimbo hilo kuelezea madai ya NCCR-Mageuzi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!