Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Madereva kuwaweka kikaangoni vigogo Udart
Habari Mchanganyiko

Madereva kuwaweka kikaangoni vigogo Udart

Spread the love

WAKATI Serikali ya mkoa wa Dar es Salaam, ikiagiza watendaji wa Mradi wa Mabasi yaendayo Haraka (Udart) kutoa sababu za kutochukua hatua madhubuti kuondoa kero ya usafiri kwa abiria, ifikapo kesho majira ya saa 12.30 asubuhi, kampuni hiyo imeeleza sababu za kero hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Udart kupitia msemaji wake, Deus Bugaywa imedai sababu za kukosekana kwa usafiri kwa abiria wa Udart hasa leo tarehe 10 Oktoba 2018 majira ya asubuhi, ni mgomo wa baadhi ya madereva kwa madai ya kupinga kucheleweshewa mishahara yao.

Bugaywa ameeleza kuwa, madereva hao wameharibu mtiririko wa magari baada ya mmoja wao kwa makusudi kuziba njia ya kutokea magari hayo, kitendo kinachohujumu Udart.

“Kawaida mabasi huanza kutoka saa 9 usiku, leo yamechelewa  kuanza kazi kwa sababu kuna gari lilienda kupaki kwenye geti la nyuma ambalo mabasi yanatokea na mhusika kutokomea kusikojulikana,” amesema Bugaywa.

Kufuatia hatua hiyo, Udart inafanya uchunguzi wa hujuma hizo kwa kushirikiana na vyombo vya dola kwa ajili ya kubaini wote waliohusika, na uchunguzi utakapokamilika watachukuliwa hatua.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!