Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Kisa bangi, bosi dawa za kulevya athibitishwa na aapishwa
Habari Mchanganyiko

Kisa bangi, bosi dawa za kulevya athibitishwa na aapishwa

Rais John Magufuli akimuapisha baada ya kumthibitisha James Kaji kuwa Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Udhibiti wa Dawa za Kulevya nchini (DCEA)
Spread the love

RAIS wa Tanzania, John Magufuli, amemwapisha James Kaji kuwa Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Kaji aliyekuwa akikaimu nafasi hiyo tangu Agosti 2019 baada ya Rogers Sianga kustaafu, ameapishwa leo Jumatatu tarehe 6 Julai 2020 Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma.

Kiapo cha Kaji kimefanyika muda mfupi baada ya Rais Magufuli kumaliza kuwaapisha wakuu wa mikoa na Katibu Tawala pamoja na kushuhudia wakuu wa wilaya wakiapishwa.

Katika hafla hiyo, Rais Magufuli akizungumza masuala mbalimbali ikiwemo operesheni aliyoifanya Kaji Wilaya ya Arumeru Mkoa wa Arusha na kukamata bangi huku akihoji viongozi wa eneo hilo kutoliona.

Rais Magufuli alisema, alimwona Kaji katika moja ta televisheni akiongoza kikosi katika kijiji cha Meru ambacho walikamata bangi.

Alisema haiwezekani Kaji atoke Dodoma aende Meru kukamata wakati eneo hilo kuna viongozi wanaopaswa kusimamia ulinzi na usalama.

Rais John Magufuli

Kutokana na hilo, Rais Magufuli pale pale akamwagiza Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Simon Sirro na Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, Diwani Athuman waliokuwepo kuwaondoa, Mkuu wa Polisi wa Wilaya hiyo (OCD), Mkuu wa Usalama wa Wilaya na wale wote wenye jukumu la kusimamia usalama kwa kushindwa kutotimiza wajibu wao.

Rais Magufuli alisema, ikiwezekana si kuwahamisha tu bali hata kuwashusha vyeo vyao.

“…na wewe (Kaji) leo naku- confirm (nakuthibitisha) kwa sababu umefanya kazi nzuri, mimi nataka mambo yaonekane, inasikitisha mpaka dawa za kulevya mtu atoke Dar es Salaam akayaone wakati mkuu wa mkoa yupo, mkuu wa wilaya yupo, ODC yupo, watendaji wengine wapo,” alisema Rais Magufuli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!