Sunday , 30 June 2024
Home Habari Mchanganyiko Watanzania waonywa kutotumia uchaguzi kuvuna hela
Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Watanzania waonywa kutotumia uchaguzi kuvuna hela

Onesmo Olengurumwa
Spread the love

WATANZANIA wametakiwa kutotumia uchaguzi kuwa wakati wa mavuno ya pesa na mali kutoka kwa wagombea, kwani kitendo hicho kinachangia nchi kupata viongozi wasiofaa kutokana na vitendo vya rushwa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Wito huo ulitolewa Jana Jumatano na Mratibu wa Kitaifa wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), Onesmo Olengurumwa, katika semina iliyoandaliwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (TAKUKURU) kujadili namna ya kudhibiti rushwa wakati wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka huu na Uchaguzi Mkuu wa 2025.

“Watanzania tunapokwenda kwenye uchaguzi tusishiriki vitendo vya rushwa, wapo watanzania wanahisi wakati wa uchaguzi ni wa kuvuna kitendo hiki kinafanya wapatikane viongozi wasiofaa, wasiokuwa na mchango wa maendeleo ya nchi na viongozi mzigo sababu wameingia madarakani kwa rushwa,” alisema Olengurumwa.

Aidha, Olengurumwa alisema TAKUKURU imeamua kutoa semina kwa mashirika yasiyo ya kiserikali (NGO’s) na asasi za kiraia kwa kuwa zinajua mchango wake katika utoaji elimu wakati wa uchaguzi na pia ziko nchi nzima.

Olengurumwa alisema THRDC imeanza kazi ya kutoa elimu ya uraia kwa wananchi kuhusu masuala ya uchaguzi, hasa juu ya namna ya kudhibiti rushwa kwa kuwaeleza athari zake katika ukuzaji wa maendeleo yao na nchi.

Naye Mwenyekiti wa Baraza la NGO’s, Dk. Lilian Badi, alisema mashirika hayo yatashirikiana na TAKUKURU katika kudhibiti vitendo vya rushwa wakati wa uchaguzi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Mpina amng’ang’ania Bashe, kumburuza mahakamani pamoja na bodi ya sukari

Spread the loveMbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina (CCM) amesema amenuia kumpeleka mahakamani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Majahazi yadakwa na madumu 1,731 ya mafuta ya kupikia

Spread the loveKikosi kazi cha Polisi Wanamaji Dar es Salaam kimekamata majahazi...

Habari za SiasaKimataifa

30 wafariki dunia maandamano Kenya

Spread the loveShirika la Human Rights Watch limesema takriban watu 30 walifariki...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa wa mauaji ya mtoto mwenye ualbino wafikishwa mahakamani

Spread the loveWATUHUMIWA wa mauaji ya Asimwe Novath, mtoto mwenye ualbino, wamefikishwa...

error: Content is protected !!