Friday , 28 June 2024
Home Habari Mchanganyiko Wanunuzi wa madini Songwe wampa tano Samia kupaisha sekta ya madini
Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wanunuzi wa madini Songwe wampa tano Samia kupaisha sekta ya madini

Spread the love

WANUNUZI wa madini ya dhahabu mkoani Songwe wamempongeza Rais Samia SuluhuHassan kwa kufanya mapinduzi ya kiuchumi katika sekta hiyo kwa kuiwezesha kupaa maradufu kimapato ikilinganishwa na miaka iliyopita. Anaripoti Ibrahim Yaasin, Songwe… (endelea).

Wakizungumza na MwanaHALISI jana Jumatano katika ofisi za madini zilizopo Mkwajuni wilayani Songwe, Mkurugenzi wa kampuni ya ununuzi wa madini, Mohammed Sharif amesema jitihada za Rais Samia pia zimewezesha kuzuia utoroshwaji wa madini.

Amesema awali walikuwa wakiwafuata wachimaji majumbani mwao kuomba wawauzie dhahabu huku wengine wakigoma wakitaka kusafirisha nje ya mkoa hali hiyo iliyowapa ugumu kupata mzigo na kuhatarisha usalama wao na fedha zao kutokana na ulinzi mdogo.

Amesema baada ya ujenzi wa soko la pamoja na kuweka bei elekezi kwenye mbao za matangazo, wamenunua dhahabu kwa urahisi na hata wachimbaji wamekuwa wakipeleka kuuza madini yao katika soko hilo hali iliyomaliza utoroshwaji wa dhahabu.

Ameongeza kutokana na mageuzi hayo, wameweza kusaidia jamii inayozunguka soko hilo katika nyanja mbalimbali ikiwamo sekta za afya, elimu, umeme, miundombinu ya barabara na kusaidia ujenzi wa nyumba za ibada ikiwemo misikiti.

Mbali na kusaidia jamii hususani kwenye ujenzi, Sharif pia amesema wamewajengea nyumba mbili wazee wasiojiweza ambazo zipo asilimia 80 za ujenzi pamoja na kutoa michango mbalimbali katika halmashauri.

Naye Said Mabruki ambaye pia ni mnunuzi wa madini, amesema kutokana na uwepo wa soko hilo la pamoja, wametoa ajira zaidi ya 60 katika kada mbalimbali kwa vijana wanaojishughulisha na uchimbaji kwa kuwapa mitaji.

Naye Mnunuzi wa madini, Fove Swaleh amesema siku za hivi karibuni Rais Samia kupitia waziri wa madini Anthony Mavunde, alitoa leseni za vitalu 19 kwa vikundi vya wachimbaji hali itakayowasaidia kukopesheka kwa kuwa watakuwa na leseni ambazo ni kama dhamana kwao.

Kwa upande wake Chonde Malembo amesema katika miaka mitatu ya uongozi wa Rais Samia hali ya kipato kwa wadau wa sekta ya madini kimeongezeka ukilinganisha na miaka iliyopita.

“Kwa sababu madini yote yanauzwa kwa bei elekezi ambayo kwa gram 1 inauzwa Sh 176,000 na wanunuzi wote wapo sehemu moja ambayo inarahisisha hata serikali kuchukua mapato yake. Pia hakuna utoroshwaji wa madini na hadi kufikia Mei mwaka huu walikusanya asilimia 71 za mapato,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Dk. Mwinyi aipa tano Oryx kwa ujenzi wa bohari ya kuhifadhia gesi Znz

Spread the loveRAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk....

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Watanzania waonywa kutotumia uchaguzi kuvuna hela

Spread the loveWATANZANIA wametakiwa kutotumia uchaguzi kuwa wakati wa mavuno ya pesa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

MNEC CCM Rukwa atofautiana na Serikali kufungwa uvuvi Ziwa Tanganyika

Spread the loveWakati Serikali ikiwa imefunga shughuli za uvuvi katika Ziwa Tanganyika...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Taifa gesi yaja na mitungi ya bei nafuu kwa wanafunzi vyuo vikuu

Spread the loveKampuni ya kuuza nishati ya gesi ya kupikia majumbani ya...

error: Content is protected !!