Sunday , 30 June 2024
Home Habari Mchanganyiko Wakuu wa nchi EAC kumchagua katibu mkuu mpya
Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wakuu wa nchi EAC kumchagua katibu mkuu mpya

Spread the love

Wakuu wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) wanatarajiwa kukutana kupitia njia ya mtandao tarehe 7 Juni mwaka huu katika Mkutano wa 23 wa Jumuiya hiyo yenye nchi wanachama nane. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa… (endelea).

Moja ya ajenda ya mkutano huo ni kupitishwa kwa Veronica Mueni Nduva kuwa Katibu Mkuu mpya wa EAC.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Afisa Uhusiano wa Mawasiliano ya Umma kutoka Jumuiya hiyo, Simon Owaka, kikao hicho, ambacho kitakuwa chini ya uenyekiti wa Salva Kiir Mayardit, Rais wa Sudan Kusini, pia kitapitisha jina la Jaji wa Mahakama ya Haki ya Afrika Mashariki (EACJ), ambaye pia anatoka Kenya.

Veronica Mueni Mwende

Serikali ya Kenya imependekeza jina la Veronica Mueni Nduva kuchukua nafasi ya Caroline Mwende Mueke katika nafasi ya Katibu Mkuu wa EAC.

Ikumbukwe kuwa, jina la Mueke lilipendekezwa na Rais wa Kenya, William Ruto kama mbadala wa Peter Mutuku Mathuki, ambaye ameteuliwa kuwa Balozi wa Kenya nchini Urusi.

Mueke alitarajiwa kumaliza kipinchi cha miaka miwili cha uongozi wa mtangulizi wake.

Hata hivyo, tarehe 15 Aprili 2024, Serikali ya Kenya ilipitisha jina la Veronica Mueni Mwende kama mbadala wa Mweke ndani ya EAC.

Kwa mujibu wa kifungu hicho cha sheria, Katibu Mkuu wa EAC, anapaswa kuhudumu kwa kipindi cha miaka mitano.

Hata hivyo, Mathuki alikuwa amehudumu kwa miaka mitatu, katika nafasi hiyo ya juu ndani ya EAC, kabla ya maamuzi ya tarehe 8 Machi 2024, yaliyofikiwa na Rais Ruto.

Kulingana na itifaki ya kuanzisha EAC, Rais wa nchi husika anaweza kupendekeza jina kwa nafasi ya Katibu Mkuu, kabla ya kuidhinishwa na Mkutano wa Wakuu wa nchi za Afrika Mashariki.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Mpina amng’ang’ania Bashe, kumburuza mahakamani pamoja na bodi ya sukari

Spread the loveMbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina (CCM) amesema amenuia kumpeleka mahakamani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Majahazi yadakwa na madumu 1,731 ya mafuta ya kupikia

Spread the loveKikosi kazi cha Polisi Wanamaji Dar es Salaam kimekamata majahazi...

Habari za SiasaKimataifa

30 wafariki dunia maandamano Kenya

Spread the loveShirika la Human Rights Watch limesema takriban watu 30 walifariki...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa wa mauaji ya mtoto mwenye ualbino wafikishwa mahakamani

Spread the loveWATUHUMIWA wa mauaji ya Asimwe Novath, mtoto mwenye ualbino, wamefikishwa...

error: Content is protected !!