Sunday , 30 June 2024
Home Habari Mchanganyiko Sugu aanza kazi Nyasa licha ya pingamizi la Msigwa
Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Sugu aanza kazi Nyasa licha ya pingamizi la Msigwa

Spread the love

MWENYEKITI mpya wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Kanda ya Nyasa, Joseph Mbilinyi (Sugu), ameanza kazi rasmi licha ya ushindi wake kuwekewa pingamizi na mtangulizi wake, Mchungaji Peter Msigwa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Kupitia ukurasa wake wa Mtandao wa X, jana Jumatano, Sugu ameandika ameongoza kikao cha kwanza cha uongozi wa Kanda hiyo.

“Leo nimeongeza kikao kazi cha kwanza Kanda ya Nyasa, viongozi wote wa juu wameshiriki yaani Makamu Mwenyekiti, Katibu na mtunza hazina pamoja na wenyeviti wa mabaraza ya Bazecha na Bavicha. Nyasa Moja,” ameandika Sugu.

Sugu ameanza kazi huku kukiwa na rufaa ya kupinga ushindi wake alioupata katika Uchaguzi wa kanda hiyo uliyofanyika hivi karibuni

Rufaa hiyo ilikatwa Jumapili iliyopita na Msigwa, ambaye alikuwa mshindani wa karibu na Sugu.

Katika Uchaguzi huo, Sugu aliyepata kura 54, alimshinda Msigwa kwa kura 2.

Msigwa amekata rufaa hiyo katika Kamati Kuu ya Chadema, akiomba matokeo hayo yafutwe Kisha uchaguzi ufanyine upya kwa madai kuwa wa awali haukuwa halali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Mpina amng’ang’ania Bashe, kumburuza mahakamani pamoja na bodi ya sukari

Spread the loveMbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina (CCM) amesema amenuia kumpeleka mahakamani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Majahazi yadakwa na madumu 1,731 ya mafuta ya kupikia

Spread the loveKikosi kazi cha Polisi Wanamaji Dar es Salaam kimekamata majahazi...

Habari za SiasaKimataifa

30 wafariki dunia maandamano Kenya

Spread the loveShirika la Human Rights Watch limesema takriban watu 30 walifariki...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa wa mauaji ya mtoto mwenye ualbino wafikishwa mahakamani

Spread the loveWATUHUMIWA wa mauaji ya Asimwe Novath, mtoto mwenye ualbino, wamefikishwa...

error: Content is protected !!