Sunday , 30 June 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali yakana kuweka rehani bahari, madini
Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali yakana kuweka rehani bahari, madini

Mobhare Matinyi
Spread the love

SERIKALI ya Tanzania, imesema haijaweka rehani rasilimali za nchi ili kupata mkopo wa zaidi ya Sh. 6.7 trilioni, kutoka katika Serikali ya Korea Kusini. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Ufafanuzi huo umetolewa leo tarehe 4 Juni 2024, jijini Dar es Salaam na Msemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi, baada ya baadhi ya vyombo vya habari vya kimataifa kudai Tanzania imetoa sehemu ya bahari na madini kama dhamana ya kupata mkopo huo.

“Labda nideme kwamba Serikali yetu haijaweka rehani kitu chochote au mali yoyote kama ilivyopotoshwa na baadhi ya vyombo vya habari na mitandao ya kinamii. Korea haijapewa sehemu ya bahari yetu mkopo huu haunaasharti yoyote ya kwueka rehani kitu chochote,” amesema Matinyi.

Matinyi amevitaka vyombo vya habari vilivyotoa madai hayo kuomba radhi akidai vimefanya upotoshaji.

“Tunatarajia waliopotosha watarekebisha na kuomba radhi wasomaji wao kwa kutoka taarifa zisizokamili au kwa kupotosha,” amesema Matinyi

Matinyi amesema mkopo huo ni wa masharti nafuu ambao utataolewa ndani ya miaka mitano. Utaanza kulipwa baada ya miaka 25 kwa muda wa miaka 40.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Mpina amng’ang’ania Bashe, kumburuza mahakamani pamoja na bodi ya sukari

Spread the loveMbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina (CCM) amesema amenuia kumpeleka mahakamani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Majahazi yadakwa na madumu 1,731 ya mafuta ya kupikia

Spread the loveKikosi kazi cha Polisi Wanamaji Dar es Salaam kimekamata majahazi...

Habari za SiasaKimataifa

30 wafariki dunia maandamano Kenya

Spread the loveShirika la Human Rights Watch limesema takriban watu 30 walifariki...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa wa mauaji ya mtoto mwenye ualbino wafikishwa mahakamani

Spread the loveWATUHUMIWA wa mauaji ya Asimwe Novath, mtoto mwenye ualbino, wamefikishwa...

error: Content is protected !!