Friday , 28 June 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali yaahidi kushirikiana na UNCDF, EU kusaidia ajenda nishati safi
Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali yaahidi kushirikiana na UNCDF, EU kusaidia ajenda nishati safi

Spread the love

Imeelezwa kuwa, Jumuiya ya Umoja wa Ulaya (EU) na washirika wengine wa maendeleo wamekuwa msaada mkubwa katika kusaidia Ajenda ya Nishati Safi ya kupikia kuzidi  kusonga mbele hapa nchini. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga wakati  akimwakilisha Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko katika warsha ya nishati safi ya kupikia iliyoanza tarehe 19 Juni 2024 jijini Dar es Salaam.

“Serikali inatambua michango ya programu mbalimbali zinazotekelezwa na washirika wa maendeleo na sekta binafsi ikiwemo ya mradi wa CookFund unaoendelea katika nchi yetu. Katika kuendeleza sekta hii, tuko tayari kuendelea kushirikiana na UNCDF na wadau wengine wa nishati safi ya kupikia,” amesema Kapinga.

Aidha, amewataka wadau kushirikiana na serikali ili kwa pamoja kutafuta na kupendekeza mikakati ambayo itaharakisha lengo la nchi la asilimia 80 ya watanzania kutumia Nishati Safi ya Kupikia ifikapo 2034.

Amesisitiza kuwa, kila mmoja ana jukumu muhimu katika kufanikisha maendeleo ya soko na teknolojia zinazohitajika kufikia lengo hilo  la asilimia 80 ya Watanzania kuhamia kwenye Nishati Safi ifikapo 2034 kama ilivyoainishwa kwenye Mkakati wa Kitaifa wa Nishati Safi ya Kupikia.

“Warsha hii ni moja ya utekelezaji wa maagizo ya Rais Samia Suluhu Hassan wakati wa uzinduzi wa Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi 2024 – 2034, ambapo aliagiza Wizara ya Nishati kukaa pamoja na wadau wa Nishati Safi ya Kupikia na kuzungumzia kuhusu itakavyoweza kufikia kwa pamoja malengo ya mkakati wa nishati safi ya kupikia,” amesisitiza Kapinga.

Vile vile, amewataka wadau katika kuelekea katika matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kuwa wabunifu, waoneshe juhudi na kudumusha ushirikiano miongoni mwa wadau wa sekta ili kufikia lengo.

Ameongeza kuwa, Serikali itaweka mazingira wezeshi ya upatikanaji wa Nishati Safi ya Kupikia kwa kila kaya ili kuimarisha afya ya umma na maendeleo endelevu katika Sekta ya mazingira na uchumi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Shirika la UNCDF nchini, Peter Malika amesema wanashirikiana na Serikali katika nyanja mbalimbali ikiwemo mfuko wa CookFund unaolenga kuimarisha Nishati Safi ya Kupikia. Amesema Nishati Safi ni fursa na biashara ambapo  aliwataka wadau mbalimbali kuichangamkia fursa hiyo kwa sasa.

Mkutano huo umewakutanisha wadau mbalimbali, wakiwemo Watunga Sera, Wadau wa Maendeleo, Wabunifu, Sekta Binafsi na Washirika wa Kimataifa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Dk. Mwinyi aipa tano Oryx kwa ujenzi wa bohari ya kuhifadhia gesi Znz

Spread the loveRAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk....

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Watanzania waonywa kutotumia uchaguzi kuvuna hela

Spread the loveWATANZANIA wametakiwa kutotumia uchaguzi kuwa wakati wa mavuno ya pesa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

MNEC CCM Rukwa atofautiana na Serikali kufungwa uvuvi Ziwa Tanganyika

Spread the loveWakati Serikali ikiwa imefunga shughuli za uvuvi katika Ziwa Tanganyika...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Taifa gesi yaja na mitungi ya bei nafuu kwa wanafunzi vyuo vikuu

Spread the loveKampuni ya kuuza nishati ya gesi ya kupikia majumbani ya...

error: Content is protected !!