Friday , 28 June 2024
Home Habari Mchanganyiko RC Chalamila: Nimeacha ubabe
Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

RC Chalamila: Nimeacha ubabe

Albert Chalamila
Spread the love

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chamalila amemthibishia Rais Samia Suluhu Hassan kuwa sasa ameacha ubabe na kuwataka viongozi wengine wa umma kuacha masuala ya ubabe. Anaripoti Faki Ubwa …(endelea).

Chalamila amebainisha hayo leo Jumanne jijini Dar es Salaam wakati akitoa salamu za mkoa mbele Rais Samia Suluhu Hassan kwenye Kongamano la Maendeleo ya Sekta ya Habari.

“Tuendelee kuwa viongozi wazuri tutakaoepukana na masuala ya kibabe. Wakuu wa Wilaya waliokuwepo hapa simameni Rais awaone Bomboko wa Ubongo na Saad Mtambule wa Kinondoni. Mheshimiwa Rais Meseji yako tumeisikia ingawa mimi nimeshaacha,” amesema Chalamila.

Kauli hiyo ya Chalamila imekuja siku chache baada ya Rais Samia kukemea tena ubabe wa wakuu wa mikoa na wilaya kutokana na kutumia vibaya mamlaka yao ya kumuweka mtu mahabusu kwa saa 48.

Rais Samia alitoa kauli hiyo tarehe 15 Juni mwaka huu wakati akipokea Ripoti ya Kamati ya Utekelezaji wa Mapendekezo ya Tume ya Haki Jinai.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Dk. Mwinyi aipa tano Oryx kwa ujenzi wa bohari ya kuhifadhia gesi Znz

Spread the loveRAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk....

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Watanzania waonywa kutotumia uchaguzi kuvuna hela

Spread the loveWATANZANIA wametakiwa kutotumia uchaguzi kuwa wakati wa mavuno ya pesa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

MNEC CCM Rukwa atofautiana na Serikali kufungwa uvuvi Ziwa Tanganyika

Spread the loveWakati Serikali ikiwa imefunga shughuli za uvuvi katika Ziwa Tanganyika...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Taifa gesi yaja na mitungi ya bei nafuu kwa wanafunzi vyuo vikuu

Spread the loveKampuni ya kuuza nishati ya gesi ya kupikia majumbani ya...

error: Content is protected !!