Rais Samia Suluhu Hassan amefanya utenguzi na uteuzi wa viongozi mbalimbali akiwamo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Joseph Constantine Mafuru ambaye uteuzi wake umetenguliwa. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Nafasi ya Mafuru imechukuliwa na Addo Missama. Kabla ya uteuzi, Missama alikuwa Afisa Mwandamizi, Ofisi ya Rais – Ikulu.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Jumamosi na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dk. Moses Kusiluka, viongozi wengine walioteuliwa ni Dk. Ashura Abdul Katunzi kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS).
Kabla ya uteuzi, Dkt. Katunzi alikuwa Afisa Udhibiti Ubora Mkuu, Shirika la Viwango Tanzania(TBS). Dk. Katunzi anachukua nafasi ya Dk. Athuman Yusuf Ngenya ambaye amemaliza muda wake.
Amnemteua Hassan Juma Mnyika kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo. Kabla ya uteuzi, Mnyika alikuwa Afisa Mwandamizi, Ofisi ya Rais – Ikulu. Mnyika anachukua nafasi ya Lain Ephraim Kamendu ambaye amestaafu.
Leave a comment