Sunday , 30 June 2024
Home Habari Mchanganyiko Mfanyabiashara mbaroni tuhuma za kumchoma moto “house girl” kisa wizi
Habari Mchanganyiko

Mfanyabiashara mbaroni tuhuma za kumchoma moto “house girl” kisa wizi

Wilbroad Mutafungwa, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro
Spread the love

MFANYABIASHARA maarufu jijini Mwanza, Christina Shiriri (Manka), anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kumchoma moto mfanyakazi wake wa ndani (House Girl), Grace Joseph, akimtuhumu kwa wizi wa fedha kiasi Cha Sh. 161,000. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Kwa mujibu wa taarifa ya Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza, DCP Wilbroad Mutafungwa, Manka alitekeleza tukio hilo tarehe 4 Juni 2024, baada ya kumwagia Grace  mafuta ya taa mwilini na kumchoma moto.

Taarifa ya Kamanda Mutafungwa imedai kuwa, baada ya Grace kuchomwa moto aliungua maeneo ya mikononi, tumboni na mapajani.

“Manka alidai kuibiwa fedha zake alizokuwa amehifadhi chumbani kwake na alipomuuliza binti yake wa kazi alikiri kuchukua fedha hizo na kuamua kumrejeshea. Baada ya kurejeshewa fedha hizo aliamua kumfanyia ukatili binti huyo kwa kumchoma moto,” imesema taarifa ya Kamanda Mutafungwa.

Kamanda Mutafungwa amesema mtuhumiwa anaendelea kuhojiwa kwa kina na atafikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika.

Kuhusu majeruhi, Kamanda Mutafungwa amesema amepelekwa katika Hospitali ya Wilaya ya Misungwi kwa ajili ya matibabu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Mpina amng’ang’ania Bashe, kumburuza mahakamani pamoja na bodi ya sukari

Spread the loveMbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina (CCM) amesema amenuia kumpeleka mahakamani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Majahazi yadakwa na madumu 1,731 ya mafuta ya kupikia

Spread the loveKikosi kazi cha Polisi Wanamaji Dar es Salaam kimekamata majahazi...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa wa mauaji ya mtoto mwenye ualbino wafikishwa mahakamani

Spread the loveWATUHUMIWA wa mauaji ya Asimwe Novath, mtoto mwenye ualbino, wamefikishwa...

Habari Mchanganyiko

Sangoma awaponza vijeba, watupwa jela maisha kwa kubaka wanafunzi

Spread the loveMAHAKAMA ya wilaya Nkasi Mkoani Rukwa, imemhukumu kifungo cha maisha...

error: Content is protected !!