Thursday , 4 July 2024
Home Habari Mchanganyiko Mbowe, Prof. Kitila ‘wavaana’
Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Mbowe, Prof. Kitila ‘wavaana’

Spread the love

MITIZAMO ya kisiasa kuhusu ugumu wa mtu kuwa mwanachama wa chama cha upinzani hususani Chadema imewagonganisha Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe na Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Prof. Kitila Mkumbo baada ya ‘kuvaana’ hadharani. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Majibizano kati ya vigogo hao yamekuja siku moja baada ya aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Nyasa na Mjumbe wa Kamati Kuu Chadema, Mchungaji Peter Msigwa kuhamia CCM.

Prof. Kitila Mkumbo

Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa X (zamani Twitter) jana Mbowe ameandika, kuwa chama cha upinzani hasa Chadema sio suala jepesi, linahitaji ujasiri wa namna ya pekee.

Mbowe amesema viongozi wengi wa upinzani na Watanzania wazalendo wa nchi hii wanapitia nyakati ngumu kutokana na uoga wa serikali ya CCM.

“Marehemu Mzee Lowassa alithubutu kuingia CHADEMA, japo baada ya muda alirudi CCM tunatambua ujasiri wa maamuzi yake.

“Kitu pekee kitakachoikoa Tanzania kutoka kwenye mikono ya watawala ni ujasiri na uthubutu wa mwananchi mmoja mmoja; tuanze sasa kulipigania taifa letu,” aliandika Mbowe.

Hata hivyo, muda mchache baada ya andiko hilo, Prof. Kitila ambaye pia ni mbunge wa Ubungo kupitia CCM, naye alijibu ujumbe wa Mbowe kwa kuandika;

“Makosa ya msingi na ya ki historia ya CDM ni mawili: 1. Kiburi cha kupendwa. 2. Kuamini makosa yao sio yao bali yanasababishwa na watu wengine nje ya CDM (externalization of your problem).

“Ujasiri wa maana kwa sasa ni kukubali kwamba makosa ni ya kwenu na kuanza kuyashughulikia. Pole sana Mr Chair,” amendika Prof. Kitila ambaye aliwahi kuwa kada wa Chadema kabla ya kufukuzwa ndani ya chama hicho kwa tuhuma za usaliti kisha kwenda kuwa mmoja wa waanzilishi wa ACT Wazalendo kabla ya kuteuliwa na Rais John Magufuli kuwa Katibu Mkuu wizara ya maji kisha kuhamia CCM.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko awataka Watanzania kulinda viumbe hai baharini

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaKimataifa

Waingereza kuifuta historia ya Conservatives leo?

Spread the loveWaingereza milioni 50 wanatarajiwa kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu leo...

Habari za SiasaKimataifa

Rais Biden agoma kujitoa uchaguzi Novemba, aangukia pua kura za maoni

Spread the loveRAIS wa Marekani, Joe Biden amekataa kujitoa kwenye uchaguzi wa...

BiasharaHabari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia, Nyusi wapongeza mkakati wa utanuzi PBZ, yakaribishwa kufungua tawi Msumbiji

Spread the loveRais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amepongeza jitihada zinazofanywa na...

error: Content is protected !!