Sunday , 30 June 2024
Home Habari Mchanganyiko Biteko aiagiza Tanesco kujenga laini mpya ya umeme Ushirombo
Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aiagiza Tanesco kujenga laini mpya ya umeme Ushirombo

Spread the love

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko ameliagiza Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kujenga laini mpya ya umeme kutoka Nyakanazi-Ushirombo na Kahama Bongwe hadi Bukombe ili kuhakikisha hali ya upatikanaji wa umeme katika  Wilaya ya Bukombe inaimarika. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Dk. Biteko ametoa agizo hilo alipozungumza na wananchi wa Jimbo la Bukombe, Mkoa wa Geita ambapo amesema kuwa sambamba na ujenzi wa laini hizo za umeme, kutajengwa kituo cha kupoza Umeme Bukombe ili kuhakikisha wananchi wakiwemo wa Ushirombo wilayani Bukombe wananufaika na umeme wa uhakika.

‘’ Umeme tunaopata Bukombe unatoka Bulyanhulu,  unapita Mbogwe na kuja  Bukombe ambapo  ukifika hapa unakuwa na nguvu hafifu na ikitokea hitilafu Bulyanhulu Bukombe pia inakosa umeme hivyo ni vema TANESCO ikajenga laini hizo mpya  ili wananchi wa Bukombe wapate umeme wa uhakika,” amesema Biteko.

Kuhusu uwepo wa umeme wa kutosha nchini, Dk. Biteko amesema  Serikali  imefanya kazi kubwa ya  kuhakikisha wanaondoa mgao wa umeme  kwa kuongeza vyanzo mbalimbali vya uzalishaji umeme na hivyo  kuondoa tatizo la kukatika mara kwa mara kwa nishati hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Mpina amng’ang’ania Bashe, kumburuza mahakamani pamoja na bodi ya sukari

Spread the loveMbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina (CCM) amesema amenuia kumpeleka mahakamani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Majahazi yadakwa na madumu 1,731 ya mafuta ya kupikia

Spread the loveKikosi kazi cha Polisi Wanamaji Dar es Salaam kimekamata majahazi...

Habari za SiasaKimataifa

30 wafariki dunia maandamano Kenya

Spread the loveShirika la Human Rights Watch limesema takriban watu 30 walifariki...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa wa mauaji ya mtoto mwenye ualbino wafikishwa mahakamani

Spread the loveWATUHUMIWA wa mauaji ya Asimwe Novath, mtoto mwenye ualbino, wamefikishwa...

error: Content is protected !!