Thursday , 4 July 2024
Home Habari Mchanganyiko DC Itunda akemea imani potofu zinazosababisha ubakaji
Habari Mchanganyiko

DC Itunda akemea imani potofu zinazosababisha ubakaji

Spread the love

VITENDO vya ubakaji, mauaji yatokanayo na visa vya wivu wa mapenzi na imani za kishirikina, vimetajwa kuwa ni moja ya changanoto zinazoikumba jamii hali inayosababisha kukithiri kwa mmomonyoko wa maadili. Anaripoti Ibrahim Yassin … Songwe, (endelea).

Kauli hiyo imetolewa jana Jumanne na Mkuu wa wilaya ya Songwe, Solomoni Itunda katika hitimisho la mkutano wa injili uliofanyika kwenye uwanja wa shule ya msingi Ichenjezwa wilayani Mbozi.

Akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo, Itunda amesema viongozi wa nyumba za Ibada na waumini wengine wana nafasi kubwa kukemea vitendo hivyo wakiwa kwenye mikutano ama madhabahuni ili jamii iishi kwa kumtegemea Mungu.

Mkutano huo ulioendeshwa na uongozi wa kanisa la New Life in Christ ambayo ni muungano wa makanisa mbalimbali ya kikristo nchini, umefanyika kwa muda wa siku saba mkoani Songwe.

Akiwasilisha salamu za Rais Samia Suluhu Hassan, Itunda ameeleza kuwa Rais Samia anatambua  kazi inayofanywa na viongozi wa dini ndiyo maana amekuwa akishirikiana nao katika mambo mbalimbali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia, Nyusi wapongeza mkakati wa utanuzi PBZ, yakaribishwa kufungua tawi Msumbiji

Spread the loveRais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amepongeza jitihada zinazofanywa na...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Bwire Mtendaji mpya DAWASA

Spread the loveMhandisi Mkama Bwire ameteuliwa kushika nafasi ya Kaimu Afisa Mtendaji...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia aahidi ushirikiano Rais mpya TEC

Spread the loveWaziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Waziri amtaka MNEC CCM Rukwa kuheshimu uamuzi wa Serikali kufunga Ziwa Tanganyika

Spread the loveNAIBU Waziri wa Mifugo na Uvivu, Alexander Mnyeti, amemtaka Mjumbe...

error: Content is protected !!