Thursday , 4 July 2024
Home Habari Mchanganyiko “Acheni kuwatumikisha watoto”
Habari Mchanganyiko

“Acheni kuwatumikisha watoto”

Spread the love

Wazazi na walezi Kijiji cha Ipapa Kata ya Ipunga Wilaya ya Mbozi mkoni Songwe wametakiwa kuacha tabia ya kuwafanya watoto vitega uchumi vya kuendesha familia na kuwakoseha haki yao ya msingi ya kupata elimu. Anaripoti Ibrahim Yassin, Songwe… (endelea).

Wito huo umetolewa jana Jumanne na Polisi Kata ya Ipunga, Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Eletisia Mtweve alipokuwa anatoa elimu ya madhara ya ajira kwa watoto  aliowakuta kijijini hapo wakifanyishwa kazi za kiuchumi ili kuendesha familia zao.

“Ajira kwa watoto inaonesha unyonyaji kwa watoto kupitia aina yoyote ya kazi ambayo inawanyima kuishi kwenye utoto wao, inawafanya washindwe kuhudhuria shule na inawaletea madhara ya kiakili, kimwili, kijamii na kimaadili” alisema Mkaguzi Mtweve

Jeshi la Polisi linaendelea kutoa elimu katika jamii kwa kuyafikia makundi mbalimbali na kuwajengea uelewa wa mambo mbalimbali yanayohusu usalama ili jamii iache matendo maovu na kuuchukia uhalifu kwa usalama wa mali zao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko awataka Watanzania kulinda viumbe hai baharini

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

BiasharaHabari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia, Nyusi wapongeza mkakati wa utanuzi PBZ, yakaribishwa kufungua tawi Msumbiji

Spread the loveRais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amepongeza jitihada zinazofanywa na...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Bwire Mtendaji mpya DAWASA

Spread the loveMhandisi Mkama Bwire ameteuliwa kushika nafasi ya Kaimu Afisa Mtendaji...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia aahidi ushirikiano Rais mpya TEC

Spread the loveWaziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza...

error: Content is protected !!